WAZIRI WA VIWANDA AKAGUA UJENZI WA KIWANDA CHA SARUJI LINDI


Waziri wa Viwanda na biashara,Abdallah Kigoda
akipata taarifa fupi ya kazi za ujenzi wa kiwanda cha Simenti toka kwa
Mkurugenzi wa Meis Industries,Merey Ally Saleh

........................................................................................................................

Na Abdulaziz,Lindi

Zaidi ya  dola milioni 30 zinatarajia kutumika kwa ajili ya ujenzi wa
kiwanda cha Lindi simenti ambacho kimeanza ujenzi wake mapema mwenzi
feb  na  kinatarajia  kumamilika baada ya miezi 14 kuanzi sasa.

Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa Meis Industries company
Ltd,, Merey Ally Saleh alipokuwa anazungumza na waziri wa viwanda na
biashara Abdala Kigoda wakati alipotembelea kuangalia maendeleo ya
ujenzi wa kiwanda hicho .

Meley alisema kukamilika kwa ujenzi wa kiwanda hicho kutasaidia
kuajiri watu zaidi ya 1000 na kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 600
hadi 700 za sement kwa siku ambayo Itasaidia wakazi wake kupata bidhaa
hiyo kwa bei nafuu kuliko hivyo sasa.


Alisema kiwanda pia kitatumia raslimali zinazopatikana  hapa nchini
kwa asilimia 95 na asilimia tano bidhaa za kutoka nje ambazo ni
kemikali za kuumulia udongo  na kufanya kuwa sementi.

Kwa upande wake waziri wa viwanda Abdalah Kigoda ameipongeza  kampuni
ya Meis kwa kitendo cha kufikiria kujenga kiwanda hicho  na kueleza
kuwa kitakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo kwa mikoa ya kusini
Lindi na Mtwara  na kupunguza tatizo la ajira lililopo.

Kigoda alisema kiwanda hicho kitakuwa cha nne kwa ukubwa ambacho
kinatumia raslimali za  ndani kwa asilimia kubwa kama vile viwanda vya
Twiga sementi, Tanga sementi na Lindi Sementi.

Alisema  serikali inaona juhudi za wawekezaji  na hivyo basi  iko
katika utaratibu wa kuondoa changamoto cha ukosefu wa umeme ambao
umekuwa kero kubwa kwa wawekezaji wa viwanda hapa nchi kwa kuharakisha
miradi ya uvunaji wa gesi kwa ajili ya nishati hiyo

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI