BREAKING NEWS...IRINGA SI SHWARI MVUTANO KATI YA MACHINGA NA POLISI WATISHIA USALAMA
Machinga wakiendelea na shughuli zao kama kawaida eneo la mashine Tatu asubuhi hii kutokana na kauli ya mbunge Msigwa kuwaruhusu kurejea ,chini polisi wakiwa eneo hilo |
Hali si shwari katika Manispaa ya Iringa baada ya
kauli mbunge wa
jimbo hilo Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) kuwataka
wafanyabiashara wadogo wadogo
(machinga) kurejea kufanya kazi katika eneo la barabara ya Mashine
tatu kutekelezwa na machinga hao.
Msigwa ambae aliitoa
kauli hiyo April 23 mwaka huu katika
mkutano wa wabunge wa chadema
waliosimamishwa bungeni
,mkutano uliofanyika katika uwanja
wa Mwembetogwa mjini hapa,kwa kuwataka Machinga kurejea
eneo hilo na iwapo mtu atafika
kuwanyanyasa basi wana----!!!?
Machinga hao leo
wameitikia kauli hiyo kwa kurejea
eneo hilo na kupelekea askari
wa kutuliza ghasia (FFU)
kutanda eneo hilo na kushindwa kutumia nguvu
zaidi ya kuwataka wafanyaiashara
hao kuendelea na shughuli zao
eneo hilo .
Comments