CHELSEA ASILIMIA 99.9 WAMEMPATA FALCAO NA WAMEAMUA KUACHANA NA CAVANI
KLABU ya Chelsea inaamini imeshinda mbio za kuwania saini ya mshambuliaji wa Atletico Madrid, Radamel Falcao.
Mazungumzo
na wawakilishi wa nyota huyo wa Colombia na viongozi wa Atletico
yamekuwa yakiendelea kwa miezi kadhaa sasa, lakini Chelsea wanafikiri
wako karibu kumsajii.
BIN ZUBEIRY kwa msaada wa Sportsmail inaweza
kuweka bayana kwamba, klabu hiyo ya London imeachana na mpango wa muda
mrefu wa kumsajili Edinson Cavani na kuongeza nguvu katika kuwania saini
ya Falcao.
Tumempata mtu wetu: Chelsea inaamini iko karibu sana kumnasa Radamel Falcao
Amefunga: Falcao akishangilia baada ya kufunga dhidi ya Sevilla kwenye La Liga Jumapili
Roman
Abramovich ameridhia kumpa mshahara wa Pauni 200,000 kwa wiki mchezaji
huyo na pia atatoa kiasi cha Pauni milioni 46 ambazo Atletico inataka
kama dau la kumuuza nyota wake huyo.
Kipa
wa Chelsea, Thibault Courtois yuko ndani ya mazungumzo ya uhamisho.
Mbelgiji huyo amekuwa kivutio akicheza kwa mkopo wa muda mrefu Atletico
na klabu hiyo ya Hispania inataka kuendelea na kipa huyo mwenye umri wa
miaka 20.
Timu
ya makocha wa Chelsea, inaamini Courtois atanufaika kutoka kwa kucheza
kwa mkopo na kurudi Ligi Kuu England msimu ujao, wakiwa wamemuandaa
kurithi mikoba ya Petr Cech.
Lakini wako tayari kumuacha kwa msimu mwingine katika Jiji la Madrid, ili wamtumie kipa huyo kama chambo cha kumnasa Falcao.
Chelsea
ilikuwa inamtaka sana Falcao, mwenye umri wa miaka 27 na kama itamkosa
ilipanga kuhamishia ndoana zake kwa Cavani, mwenye umri wa miaka 26.
Nyota huyo wa Uruguay amekuwa kipenzi cha mmiliki wa Chelsea, Abramovich
na Mkurugenzi wa Ufundi, Michael Emenalo.
Wawakilishi
wa mshambuliaji huyo wa Napoli hivi karibuni walizungumza na viongozi
wa Chelsea juu ya uhamisho wa mwishoni mwa msimu, kuonyesha kwamba
Stamford Bridge yangekuwa maskani mapya ya Cavani akihamia England.
Lakini
pamoja na Chelsea kuamua kuelekeza nguvu zao kwa Falcao, pia
wanamuwania mshambuliaji wa Bayer Leverkusen, Andre Schurrle, mwenye
umri wa miaka 22.
Wakati
huo huo, Nahodha John Terry anatumai kuanza mazungumzo ya mkataba mpya
mwishoni mwa msimu. Beki huyo mwenye umri wa miaka 32, ambaye maisha
yake yote ya soka amekuwa Stamford Bridge, anamaliza mkataba wake msimu
ujao.
katikati
ya dili: Kipa wa Atletico Madrid, Thibaut Courtois, yupo kwa mkopo
kutoka Chelsea, ni sehemu ya mazungumzo ya uhamisho wa Falcao
Wameachana naye: Chelsea imeachana na mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Napoli, Edinson Cavani
Kifaa kuelekea darajani: Chelsea imepiga hatua katika mazungumzo yake na nyota wa Bayer Leverkusen, Andre Schurrle
.
Mkataba mpya? John Terry mkataba wake wa sasa Chelsea unaisha msimu ujao
Comments