HAYA NI MAUZA UZA YA KARNE IRINGA , MJANE AKIMBIA NYUMBA KWA MAUZA UZA YA MOTO KUWAKA MARA KWA MARA
Mali mbali mbali zilizoteketea na kutupwa hapa zikiwa mkaa |
Diwani wa kata hiyo ya Kwakilosa Hamza Ginga akiwa ameshika mkoba wa mjane huyo uliopotea pamoja na madaftari ya watoto kimiujiza |
Hiki ni kitanda kilichoungua kimiujiza na moto huo |
Hili ni paa la nyumba hiyo inayoungua kimiujiza kwa zaidi ya mara tano sasa kama inavyoonekana ikiwa salama salimini |
Mwanamke Bi. Faraja Chengula (31) na watoto wake akiwa na familia yake pamoja na diwani wa kata ya Kwakilosa mheshimiwa Hamza Ginga na baadhi ya viongozi wa mtaa huo wa Beila baada ya mali katika nyumba yake kuteketea kwa moto wa miujiza .
Majane Bi Faraja Chengula
........................................... HUJAFA hujaumbika bado ni kauli ya mwanamke mkazi wa mtaa wa Beila kata ya Kwakilosa katika Manispaa ya Iringa Bi. Faraja Chengula (31) ambae amelazimika kuikimbia nyumba aliyopanga na kwenda kuomba hifadhi kwa kiongozi mmoja wa kidini kama njia ya kujinusuru na mauza uza haya moto kimiujiza umeendelea kumtesa kwa kuteketeza mali mbali mbali bila kuleta madhara kwa binadamu.
Akizungumza na mtandao huu
wa www.francisgodwin.blogspot.com
leo mwanamke huyo ambae
ni mjane aliyepoteza mwenzi wake kwa zaidi ya miaka mitatu
sasa alisema kuwa mauza uza hayo ndani ya chumba chake yalianza toka jumatano ya April 17 mwaka huu baada ya
kurejea nyumbani na kupatwa na
wakati mgumu kutafuta ufunguo wa nyumba ambao ulipotea katika
mazingira tata.
Bi. Chengula
alisema kuwa mbali ya kupotea
ufunguo huo bado aliendelea
kushuhudia mauza uza mbali mbali
ikiwa ni pamoja na kuibuka kwa moto ambao chanzo chake bado kufahamika na
mbaya zaidi moto huo ulikuwa unawake katika
kitanda bila kuteketeza
godoro na baada ya kuuzima kwa maji bado uliibuka moto mwingine katika mito ya makochi aliyokuwa ameiweka nje
ya chumba hiyo.
“ Kweli nashindwa
kuelezea ila nilishangazwa zaidi
baada ya kuona mito hiyo ya
makochi iliyokuwa nje ya
chumba ghafla ikiwa ndani ya chumba na kuwaka moto huku
nikishuhudia moto huo ukishika kasi na hata nilipojaribu kuzima kwa maji ilishindikana “
Hata hivyo alisema
kuwa hadi sasa bado
hajatambua miujiza hiyo
inatokana na nini kwani toka mume
wake amefariki dunia ni
zaidi ya miaka miwili sasa na hakuna jambo lolote kama hilo ambalo
limepata kujitokeza na kuwa mbaya
zaidi mazingira ya moto
huo yamekuwa wakimshangaza kila mkazi wa nyumba hiyo yenye wapangaji
zaidi ya 10 pamoja na majirani wanaozunguka nyumba hiyo.
Bi.Chengula
alisema kuwa wakati mwingine
amekuwa akizikuta nguo zake
na za
watoto wake wawili
chooni na baada ya kurejea ndani
ya chumba hicho amekuwa akizikuta zikiwa ndani na mara nyingine moto huo umekuwa
ukiwaka katika eneo la sokte ya umeme bila
sokte hiyo ya plastick kuguswa na
moto huo .
“Kweli nashindwa
kujua chanzo cha mambo haya kwa
sijala kituo cha mtu yeyote na mimi ni mlokole ninayesali kanisa la
Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Mlandege na mbali ya kufanya
maombi kanisani ila bado mambo haya yameendelea
kuniandama na zaidi ya mara tano
sasa moto unawake ndani ya chumba
changu pekee “
Aidha alisema kutokana na mauza uza hayo kuchukua kasi
alilazimika kuwaita waumini wenzake na kufanya maombi katika chumba
hicho ila wakati wakiendelea kufanya maombi ghafla walijikuta
simu za viganjani zikiwa
zimepotea katika mazingira yenye utata na hadi sasa
simu hizo hazijapatikana.
Pia alisema kuwa juzi
katika mazingira tata madaftari
ya wanafunzi yaliyokuwa katika mfuko ,mkoba wake
wa mkononi uliokuwa na vitu mbali mbali
pamoja na pea moja ya viatu
vyake vilipotea katika mazingira tata ila
leo April 26 majiar ya saa 2 asubuhi
baada ya viongozi wa
serikali ya mtaa na diwani kufika
eneo hilo wakiwa na mwandishi wa habari
hizi vitu hivyo vilionekana eneo ambalo
ni jeupe sana pamoja na kuwepo kwa
umande katika eneo hilo ila vitu hivyo havikugusa hata tone la umande.
Balozi wa mtaa
huo wa Beila Bi. Christina Ndale alisema kuwa
nyumba hiyo ambayo imekuwa ikiandamwa na mauza uza hayo ni nyumba Block ‘Y’
79 na kuwa wao kama mtaa wamepata
kushuhudia mauza uza hayo nab ado wanaumiza
vichwa kujua chanzo cha mambo hayo .
Wakati
mwenyekiti wa mtaa huyo Alan Koma koma alisema
kuwa mauza uza kama hayo si mara
ya kwanza kujitokeza katika mtaa huo
kwani kwa upande wake pia mambo kama hayo yalipata kumtokea kwa
nyumba yake kupigwa mawe usiku kucha
na watu
wasiofahamika mbali ya kulindwa na askari polisi
na wananchi kuzunguka nyumba hiyo kwa ulinzi wa sungusungu ila bado mawe hayo ambayo yalikuwa
yakimwagika kama mvua kutoka
angani yaliendelea kushambulia nyumba
hiyo .
Hivyo alisema
suala hilo la mauza uza ni miongoni mwa mambo ambayo yanawatesa wakazi
wa eneo hilo hivyo kuwaomba watu
wanaojihusisha na imani za
kishirikina kwa ajili ya kuwatesa wengine
kuachana na masuala hayo.
Diwani wa kata ya
Kwakilossa mheshimiwa Hamza Ginga akithibitisha kutokea kwa matukio hayo alisema kuwa yeye kama diwani anashindwa kujua
sababu kuu ya mambo hayo japo ana
mpango wa kuitisha mkutano ili kukutana na wananchi wake
wote kama njia ya kumaliza mauza
uza hayo.
Mheshimiwa Ginga
alisema kwa sasa wanakusudia
kuwaita viongozi wa dini
waliopo mjini Iringa kutoka nchini
Kenya , Uganda na mwenyeji wao askofu wa kituo cha maombezi na uponyaji cha
Overcomers Power Center Dkt Boaz Sollo
ali kufanya maombi maalum katika nyumba
hiyo na kumtaka mwamake huyo kutoukimbia mtaa kutokana na mauza uza hayo
kwani hata kama atahama kama kuna mtu anamfuatilia ataendelea kufanya hivyo.
MWISHO
|
Comments