RONALDO AIPELEKA REAL NUSU FAINALI ULAYA, ILA DROGBA, SNEIJDER BADO MOTO


WABABE wa Hispania, Real Madrid wamefuzu kutinga Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya licha ya jana usiku kufungwa 3-2 Galatasaray nchini Uturuki katika mchezo wa marudiano wa Robo Fainali.
Kwa matokeo hayo, kikosi cha Jose Mourinho kimesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 5-2, baada awali kushinda 3-0 katika mchezo wa kwanza nchini Hispania.
Jana Cristiano Ronaldo alikuwa wa kwanza kufunga bao dakika ya saba, lakini Emmanuel Eboue akaisawazishia Gala dakika ya 57, kabla Wesley Sneijder hajawafungia wenyeji bao la pili dakika ya 70.
Life in the old Drog yet: Didier Drogba was among the scorers as Galatasaray won the second leg
Utu uzima dawa: Didier Drogba alikuwa mmoja wa wafungaji wa mabao ya Galatasaray jana

Dakika mbili baadaye, Did Drogba akafunga bao la tatu, kabla ya Ronaldo kufunga tena dakika ya 90 na kuiweka sawa barabarani Real katika mbio zake za kukimbilia taji la 10 Ulaya.
Katika mchezo huo, kikosi cha Galatasaray kilikuwa: Muslera, Eboue/Elmander dk80, Zan, Kaya, Riera, Altintop/Amrabat dk46, Felipe Melo, Inan, Sneijder, Bulut /Sarioglu dk63 na Drogba.
Real Madrid: Diego Lopez, Essien/Arbeloa dk31, Pepe, Varane, Fabio Coentrao, Khedira, Modric, Di Maria, Ozil/ Albiol dk81, Ronaldo na Higuain/Benzema dk73.
Keeping the dream alive: Drogba celebrates after making it 3-1 on the night

Shangwe za bao: Drogba akishangilia baada ya kufunga bao la tatu
It all started so well: Ronaldo celebrates putting Real 1-0 up on the night
Ronaldo akishangilia baada ya kufunga bao la kwanza
Back in the game: Emmanuel Eboue scored to make it 1-1
Drogba akimpongeza ndugu yake, Emmanuel Eboue kuisawazishia Gala jana
Ahead on the night: Galatasaray's Wesley Sneijder puts his side ahead on the night
Wesley Sneijder akishangilia bao lake
The comeback is on: Sneijder gives his side hope
That should do it: Ronaldo scores at the death to secure Real's passage
Ronaldo akishangilia bao lake la pili jana
Into the semi: Real Madrid's Jose Mourinho shakes hands with Fatih Terim after the game
Kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho akipeana mikono na kocha wa Gala, Fatih Terim baada ya mechi

Katika mchezo mwingine jana, Borussia Dortmund ilifanikiwa kushinda 3-0 dhidi ya Malaga kwenye Uwanja wa Signal Iduna Park, hivyo kufuzu kwa ushindi wa jumla wa 3-2, baada ya awali kufungwa 2-0 Hispania.
Back from the brink: Borussia Dortmund completed a stunning comeback with two goals in injury time Borussia Dortmund wakishangilia ushindi wao jan

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.