TORRES AIPELEKA CHELSEA NUSU FAINALI ULAYA, SPURS NA NEWCASTLE NJE
MATOKEO YOTE EUROPA LEAGUE JANA: (Gonga usome chini)
KOCHA Andre
Villas-Boas amewaita wachezaji wa timu yake ‘mashujaa’ usiku wa jana
baada ya kutolewa kwa mikwaju ya penalti 4-1 baada ya sare ya 2-2 ndania
ya dakika 120 iliyofanya sare ya jumla ya 4-4 katika Europa League
dhidi ya wenyeji Basle.
Ulikuwa ni
mkwaju wa penalti wa Marcelo Diaz’ ulioipeleka Basle Nusu Fainali katika
mechi yao ya 19 ya mashindano yaliyoanza Julai mwaka jana. Lakini
ilikuwa zaidi ya ajabu kwa Tom Huddlestone na Emmanuel Adebayor wote
kukosa penalti zao.
Clint Dempsey
aliifungia Spurs mabao mawili katika dakika za 23 na 82, lakini Mohamed
Salah akafunga dakika ya 27 na Aleksandar 49 na kufanya sare ya 2-2.
Spurs
iliwakosa Gareth Bale, Aaron Lennon, Jermain Defoe na William Gallas
katika mchezo huo waliokuwa wakisaka ushindi wa kwanza ugenini Ulaya
dhidi ya timu ambayo haikuwa imefungwa hata bao moja nyumbani tangu
Oktoba. Kadi nyekundu ya moja kwa moja aliyopewa Jan Vertonghen pia
iliigharimu Tottenham, ingawa Spurs pamoja na yote haijashinda mikwaju ya penalti tangu mwaka 1994.
Katika mikwaju ya penalti, Schar alianza kufunga, Huddlestone akakosa, Streller akafunga (2-0), Sigurdsson akafunga (2-1), Fabian Frei akafunga (3-1), Adebayor akakosa (3-1) na Diaz akamaliza kwa kufunga pia (4-1).
Kikosi cha
Basle kilikuwa: Sommer, Philipp Degen, Schar, Dragovic, Park, El-Nenny,
Fabian Frei, Die/Diaz dk58, Salah/Alexander Frei dk111,
Stocker/Steinhofer dk70 na Streller.
Tottenham: Friedel, Walker, Dawson, Vertonghen, Naughton/Assou-Ekotto dk78, Dembele/Carroll dk59, Parker/Huddlestone dk77, Holtby, Dempsey, Sigurdsson na Adebayor.
Nje: Spurs wakimuangalia Emmanuel Adebayor akikosa penalti
Katika mchezo
mwingine, kocha Rafa Benitez alitoka uwanjani kwa furaha usiku wa jana
alipoiwezesha Chelsea kusonga mbele licha ya kufungwa mabao 3-2 ugenini
Rubin Kazan.
Chelsea imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 5-4, baada ya awali kushinda 3-1 nyumbani.
Mabao
ya Chelsea jana yalifungwa na Fernando Torres dakika ya tano na Victor
Moses dakika ya 55, wakati Kazan walipata mabao yao kupitia kwa Marcano dakika ya 51, Karadeniz dakika ya 62 na Natcho kwa penalti dakika ya 75.
Kikosi
cha Chelsea jana kilikuwa;Cech, Azpilicueta, Luiz, Terry, Ake,
Ferreira, Benayoun/Oscar dk77, Ramires/Mikel dk 60, Lampard/Ivanovic
dk90, Moses na Torres.
Rubin Kazan:
Ryzhikov, Kuzmin/Kaleshin dk45, Ansaldi, Cesar Navas, Marciano,
Orbaiz/Dyadyun dk66, Natcho, Kasaev/Ryazantsev dk72, Karadeniz, Eremenko
na Rondon.
Shujaa wa Mask: Fernando Torres akishangilia bao lake muhimu jana
Newcastle
ililazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Benfica ye Ureno, hivyo kutolewa
kwa jumla ya mabao 4-2, baada ya awali kufungwa 3-1 ugenini. Bao la
Newcastle lilifungwa na Papiss Cisse dakika ya 71 na Benfica lilifungwa
na Salvio dakika ya 90.
Comments