BARNABA, KIDUMU KUPAMBA MATEMBEZI YA HISANI 'STEP AHEAD WALK 2013
Msanii machachari wa Bongo Flava, Barnaba,
akizungumza wakati wa uzinduzi wa Matembezi ya Hisani ya 'Step Ahead Walk 2013,'
yatakayopambwa na kibao chake kiitwacho Wanawake alichoimba kwa ushirikiano na
Mrundi anayefanyia shughuli za muziki nchini Kenya, Jean Pierre Nimbona
'Kidumu.'
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na
Mahusiano wa Barclays, Tunu Kavishe, akizungumza na waandishi wa habari (hawao
pichani), wakati wa uzinduzi wa Matembezi ya Hisani ya Step Ahead Walk 2013
yatakayosindikizwa na Barnaba na Kidumu.
DAR ES SALAAM, Tanzania
'Step Ahead Walk’ ni mkakati endelevu wa Benki ya
Barclays, ambao kusudi lake ni kujenga uelewa wa kusaidia mahitaji muhimu katika
jamii. Matembezi hayo ya kila mwaka, yalizinduliwa mwaka 2008 hapa nchini na
kusaidia kuelimisha jamii kuhusu uchangishaji fedha ili kusaidia masuala ya
uzazi na afya ya watoto
KIBAO cha ‘Wanawake,’ kilichoimbwa na nyota Bongo Flava
Barnabas Elias, akishirikiana na Mrundi Jean Pierre Nimbona ‘Kidumu,’
kimezinduliwa rasmi leo na kutangazwa kupamba Matembezi ya Hisani ya ‘Step Ahead
Walk 2013,’ yanayoratibiwa na Benki ya Barclays
Tanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi huo,
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano wa Barclays, Tunu Kavishe, alisema
maudhui ya wimbo huo ni kuhamasisha wadau kujitokeza kwa wingi kushiriki ‘Step
Ahead Walk’ ambayo lengo lake ni kuchangisha pesa kwa ajili ya kinamama na
watoto wachanga.
Aliongeza kuwa, tukio hilo litafanyika Juni 8, 2013,
katika hoteli ya Golden Tulip, likihusisha matembezi ya hisani ya kilomita tano,
ambapo kila mtu katika jamii anakaribishwa kushiriki kwa kununua tiketi kwa
silingi za Kitanzania 5,000 ambazo zinapatika katika matawi ya Benki ya Barclays
kuanzia Aprili 29.
“Mwaka 2011, Benki ya Barclays na washiriki wake
walifanikiwa kukusanya shilingi mil. 150 kutokana na mauzo ya tiketi na matoleo
mengine kutoka kwa wafadhili, lakini mwaka huu lengo ni kuchangisha mara mbili
ya kiasi hicho kutoka kwenye matoleo ya washirika muhimu na washiriki wengine
katika jamii,” alisema Kavishe.
Alibainisha kuwa, kiasi kitakachochangishwa mwaka huu
kitakwenda kusaidia katika masuala ya uzazi na afya ya watoto, ikiwamo Mafunzo
kwa wakunga wa uzazi, matibabu ya Fistula na upasuaji kwa watoto waliozaliwa na
ulemavu unaosababishwa na uzazi.
‘Step Ahead Walk’ ni mkakati endelevu wa Benki ya
Barclays, ambao kusudi lake ni kujenga uelewa wa kusaidia mahitaji muhimu katika
jamii. Matembezi hayo ya kila mwaka, yalizinduliwa mwaka 2008 hapa nchini na
kusaidia kuelimisha jamii kuhusu uchangishaji fedha ili kusaidia masuala ya
uzazi na afya ya watoto.
Kavishe alisisitiza kuwa,
‘Step Ahead Walk 2013’ itafanikiwa, kama tu itawezeshwa na kila mshiriki na
jamii nzima ya Kitanzania, kwa hiyo akawataka wadau kujiunga katika matembezi
hayo ili kuweza kuleta mabadiliko katika masuala ya afya ya Uzazi na Mtoto kwa
ujumla hapa Tanzania.
Comments