BREAKING NEWS.....IRINGA NI SHWARI MACHINGA WAPINGA KUTUMIKA KISIASA ,RC IRINGA AWAPONGEZA MACHINGA KWA KUREJEA MLANDEGE
Baadhi ya maduka eneo la Mashine
tatu mjini Iringa yakiwa yamefungwa kwa hofu ya kutokea vurugu
,ambazo hata hivyo hazijatokea baada ya machinga kugoma kutumiwa
kisiasa
Hali ilivyo eneo la Mashine tatu mjini Iringa
Haya ni maadishi yanayosomeka HATARI
yaliyochorwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana kama sehemu
ya kuwatisha wananchi na kuhamasisha vurugu kabla ya jeshi la
polisi kuweka ulinzi mkali eneo hilo
Wafanyabiashara wa maduka ya mchele eneo la mashine tatu wakiendelea na biashara zao kwa utulivu zaidi leo
Hili ndilo eneo la mashine tatu kama
linavyoonekana mchana huu baada ya machinga kukubali kuheshimu sheria
ya mipango miji na kuachana na mvutano usio na tija kwao
Amani na utulivu warejea eneo la
Mashine tatu mjini Iringa ,wananchi waendelea na shughuli zao kama
kawaida leo ,machinga wakubali kutii sheria
Askari wa FFU akiwa katika ulinzi eneo la mashine tatu leo ambapo hali imetulia zaidi
Askari wa FFU mjini Iringa akipita
eneo la mashine tatu ambako machinga walipanga kufanya biashara na
vurugu leo ila hali ya amani imetawala zaidi eneo hilo
Askari wa FFU wakiwa kazini leo eneo la mashine tatu
Ulinzi waimarishwa eneo la mashine tatu ,machinga wakubali kufanya biashara eneo la Mlandege kama awali
Hivi ndivyo hali ilivyo eneo la mashine tatu leo ni amani na utulivu kwenda mbele hakuna mabomu leo
Leo ni amani zaidi Iringa hakuna vurugu zozote
Hali ya amani na utulivu imerejea
mjini Iringa baada ya machinga kukubali kuendelea na biashara zao
katika eneo la Mlandege ambalo uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya
Iringa iliwatengea wamachinga hao .
Uchunguzi uliofanywa na mtandao huu
wa www.matukiodaima.com katika eneo hilo umeshuhudia kuwepo kwa amani
zaidi na wafanyabiashara waliokuwa wamefunga maduka yao kuhofia
amani kuvurugika wameonekana wakifungua maduka yao huku machinga
ambao walihamasishwa na mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter
Msigwa (Chadema) kurejea eneo hilo wakionyesha kupuuza ushauri huo
wa mbunge na kuelekea Mlandege kama Manispaa ilivyowataka .
Baadhi ya machinga wamesema kuwa
suala hilo la machinga kurudi eneo hilo lipo kisiasa zaidi na kuwa
kama si mbunge kuwahamasisha machinga hao kupitia mikutano yake
hakuna machinga ambae angerejea eneo hilo kwani wengi wao kuwepo
Mlandege walionyesha kukubali .
Hata hivyo machinga hao wamesema
kuwa hata waliofanya vurugu wiki iliyopita si machinga ni wahuni
kutoka maeneo mbali ambali ambao walifanya fujo hizo na kuwa machinga
kama machinga hana nafasi ya kufanya vurugu zaidi ya kutafuta pesa.
Pia uchunguzi unaonyesha jeshi la
polisi mkoa wa Iringa kujipanga vema kwa siku ya jana usiku na leo
ikiwa ni pamoja na kuwakamata baadhi ya watu ambao walikuwa wakitoa
kauli za kichochezi katika vijiwe mbali mbali .
Huku askari wa FFU kwa mara ya kwanza
usiku wa kuamkia leo walionekana wakiweka ulinzi mkali katika maeneo
mbali mbali ya mji likiwemo eneo la soko la Kihesa ,Mlandege, Mashine
tatu na maeneo mengine mengi hali iliyopelekea vikundi vya vurugu
kutoweka ghafla mjini Iringa na wale waliokuwa wamepanga kuvuruga
amani kuamua kusitisha mpango huo.
Wakati huo huo mkuu wa mkoa wa Iringa
Dkt Christine Ishengoma amewapongeza machinga kwa kukubali kurejea
eneo la Mlandege ambalo uongozi wa Manispaa ya Iringa ulikuwa
umewapangia na kuwa hekima iliyoonyeshwa na machinga hao inapaswa
kuigwa na makundi mengine ambayo yamekuwa yakichochewa kufanya vurugu
kutokana na matatizo yao.
"Kweli napenda kuwapongeza sana
machinga wametumia busara sana baada ya kikao chao na mstahiki meya
wa Manispaa ya Iringa kuhusu kutafuta suluhu lao .....bila shaka
wameonyesha kumsikiliza na kumheshimu vema meya na mimi kama mkuu
wa mkoa nawaahidi kuwa suala lao litatafutiwa uvumbuzi wa kudumu
nawaomba wawe na subira na kuepuka kutumiwa na wana siasa katika
suala lao"
MWISHO
Comments