Ni ijumaa nyingine tena. Kama kawaida yetu ni wakati wa kupumua kidogo na kutafakari yaliyojiri na kupanga yajayo hata kama hatuna uwezo kamili wa kujua yatakuwaje.Ni mipango tu.Bila mipango hakiendi kitu.Ni wakati mwingine wa burudani. Leo tunayo heshima kubwa kumkumbuka Hayati Freddy Supreme Ndala Kasheba(pichani). Huyu ni miongoni mwa magwiji wa muziki ambao Tanzania imewahi kuwa nao.
Wimbo unaitwa Dunia Msongamano. Ndala Kasheba hapa alikuwa na kundi zima la Orchestra Safari Sound. Ujumbe uliomo ndani ya wimbo huu, kama binadamu yoyote akiuzingatia, ni wazi kwamba kuna mambo fulani fulani ambayo atayaepuka.Migongano mbalimbali tuliyonayo wanadamu, kuanzia kimawazo mpaka kivitendo ni kwa sababu wengi huwa tunasahau kwamba kila mtu ana akili zake.Kizuri kwangu, kibaya kwako na mambo kama hayo.
Hapo chini ni baadhi tu ya maneno kutoka kwenye beti za kwanza kwanza za wimbo Dunia Msongamano. Zisome kwanza kisha bonyeza player hapo chini uusikilize wimbo wenyewe. Ijumaa Njema. R.I.P Ndala Kasheba.

DUNIA MSONGAMANO
Mawazo yamenijia leo,
Ya Mzee wangu alokuwa akisema,
Dunia ni msongamano wa watu wenye akili tofauti,



Ukitaka kuishi vema fikiri kabla ya kujibu,
Jifunze kwa walimwengu, na walimwengu wajifunze kwako,
Dunia ni kuona mambo,
Na halafu kuyasahau

Wengine hupendelea kufurahia,
Wanaposikia fulani kafa,
Kufa kwa binadamu hupangwa na Mungu,
Namuomba Mwenyezi anipe maisha ooh

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.