Hotel ya DoubleTree by Hilton Tanzania watoa msaada wa taa 200 kwa shule za Msingi Songea - Ruvuma.
Waziri
wa Mazingira Dk. Terezya Huvisa ambaye ni Rais wa Mawaziri wa Mazingira
Barani Afrika akiipongeza Hoteli ya DoubleTree by Hilton kwa kuona
umuhimu wa elimu kwa kukabidhi taa mia mbili kwa Shule za Msingi
zilizopo manispaa ya Songea mkoani Ruvuma , Shule zilizopewa msaada huo
ni Shule ya msingi Mletele, Mwanamonga, Liumbu na Namang'ula , Taa hizi
zinazotumia Nishati ya jua pia ni rafiki wa mazingira. " Taa hizi
zitawasaidia kuepeuka kutumia vibatari na mishumaa muda wa kujisomea kwa
sababu ni hatari kwani vimekuwa vikisababisha majanga ya kuungua kwa
watoto wengi nchini ".
Mkuu
wa wilaya ya Songea Bw. Joesph Joseph Mkirikiti alie kaa katikati na
kutoka kulia kwake ni Mkurugenzi wa kanda ya Africa mashariki wa Hoteli
za DoubletTree by Hilton Tanzania Bw. Judd Helman na alie kaa kushoto
ni mkurugenzi wa Masoko Hoteli ya DoubleTree by Hilton Florenso
Kirambata wakati wa hafula ya kukabidhi msaada wa taa zinazotumia
nishati ya jua.
Mkuu wa wilaya ya Songea Bw. Joseph
Joseph mkirikiti akiteta jambo na mkurugenzi wa Masoko Hoteli ya
DoubleTree by Hilton Florenso Kirambata (kushoto) juu ya matumizi ya
taa zinazotumia nishati ya Jua ambazo pia ni rafiki wa mazingira kwa
Wanafunzi wa darasa la Saba. Kulia ni Mkurugenzi wa kanda ya Africa
mashariki wa Hoteli za DoubletTree by Hilton Tanzania Bw. Judd Helman.
Toka kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko
Hoteli ya DoubleTree by Hilton Florenso Kirambata akiwa ameshikilia taa
na wakatikati ni mkuu wa wilaya ya Songea Bw. Joseph Joseph mkirikiti
akiwa ameshikilia taa na wa mwisho ni Mkurugenzi wa kanda ya Africa
mashariki wa Hoteli ya DoubletTree by Hilton Bw. Judd helman.
Mkurugenzi
wa kanda ya Africa mashariki wa Hoteli ya DoubletTree by Hilton Bw.
Judd helman akimkabidhi moja ya taa inayotumia nishati ya Jua mwanafunzi
wa Shule ya Msingi Liumbu iliyopo ndani ya manispaa ya Songea mkoani
Ruvuma .
Waziri wa Mazingira Dk. Terezya
Huvisa ambaye ni Rais wa Mawaziri wa Mazingira Barani Afrika hapa ni
umati wa wanafunzi (Viongozi wa leo) kila mmoja akitaka ampe mkono wa
pongezi baada ya kumalizikla hafla ya kukabidhi taa za nishati ya jua
kwa shule nne za manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.
Wanafunzi toka katika shule nne za
msingi Mletele, Mwanamonga, Liumbu na Namang'ula na wakifatilia kwa
makini hutuba iliyokuwa ikitolewa kabla ya kukabidhiwa taa zinazotumia
Nishati ya jua ambazo zimetolewa na Hoteli ya DoubleTree by Hilton.
Wanafunzi hao wameishukuru Hoteli
hiyo na kusema taa hizo zitawasaidia kujisomea hata kipindi ambacho
Umeme umekatika majumbani hivyo kuongeza uwezo wao kielimu na kupunguza
matumizi ya kununua mafuta ya taa kwa ajili ya kusomea.
Naye Mkurugenzi wa Masoko Hoteli ya DoubleTree by Hilton Florenso Kirambata amesema
"tumeamua kufanya kampeni hii ambayo
ni endelevu tutakuwa tukigawa taa 200 za mezani zenye kutumia nishati
ya jua kwa wanafunzi wa darasa la saba kwa shule tofauti kila mwezi,
lengo likiwa nikuwafanya wawe na ufahamu zaidi juu ya chanzo kingine cha
umeme ambacho ni rafiki wa mazingira vile vile tunaomba wahisani
wengine nao wajitokeze".
Picha na habari kwa hisani ya www.demashonews.blogspot.com
You might also like:
Comments