Mama Kikwete awataka wazazi kutobagua watoto wao katika ufanyaji wa kazi za nyumbani
Na Anna Nkinda – Maelezo
Wazazi nchini wametakiwa kuwafundisha watoto wao kazi zote za nyumbani
bila ya kuwabagua kwamba hawa ni watoto wa kike na hawa ni watoto wa
kiume hiyo itawasaidia kuweza kujitegemea hasa wanapokuwa katika
mazingira ya tofauti na nyumbani.
Wito
huo umetolewa leo na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alipotembelea ofisi
za makao makuu ya Chama cha Girls Guide zilizopo Mwananyamala jijini
Dar es Salaam.
Mama
Kikwete ambaye pia ni Mlezi wa chama hicho alisema kuwa hivi sasa
wanawake wanatakiwa kuondokana na mfumo dume kuwa ukiwa na watoto wa
kike na wa kiume ndani ya nyumba kazi zote zinatakiwa kufanywa na mtoto
wa kike pekee.
“Mzazi
unatakiwa kuhakikisha kuwa watoto wako bila ya kuangalia jinsia
wanafanya kazi sawa sawa kama ni kupika leo iwe zamu ya huyu na kesho
zamu ya mwingine hii itamsaidia mtoto wa kiume akienda shule ya bweni
kukumbuka kuwa nyumbani nilikuwa naosha kikombe, nadeki nyumba, nafua
nguo, nashona kifungo na kuweza kufanya mwenyewe.
Lakini
leo hii mtoto wa darasa la saba hawezi kufanya kazi yoyote ya nyumbani
kwani hata mama yake naye hana muda wa kumfundisha”, alisema Mama
Kikwete.
Alisema
kuwa kama wakiwafundisha watoto vizuri kutokana na muongozo uliopo
katika madarasa ya boy skauti na girl guide watakuwa wamewakomboa hata
kama siyo wote lakini wale wachache ambao hawakupata mafunzo nyumbani
watapata mazingira ambayo yatawasaidia kujitegemea katika maisha yao.
Kwa
upande wake Grace Makenya ambaye ni mdhamini wa Chama alimshukuru Mama
Kikwete kwa kuwatembelea na kusema kuwa watoto wengi ambao ni wanachama
wa gilrs uides wameweza kufanya vizuri katika mitihani yao ya darasa la
saba na wanawake walioolewa wameweza kuzitunza ndoa zao vizuri hii ni
kutokana na mafunzo wanayowapatia.
Makenya
alisema kuwa miradi waliyonayo ni jiko la kutumia mionzi ya jua,
hosteli kwa shule za Sekondari za kutwa na mradi wa lishe bora kwa
watoto wenye utapiamlo, afya ya uzazi na maambukizi mapya ya Virusi Vya
Ukimwi (VVU), mimba zisizotarajiwa kwa wasichana wadogo na utoaji wa
elimu ya Ukimwi kwa jamii.
Chama
hicho ambacho kimeenea Dunia nzima hapa nchini kilianza mwaka 1928
huku kikiwa na dira ya kuwa na wasichana ambao wanauelewa wa matukio ya
kitaifa na ulimwengu, wenye kujiamini na kujitegemea na kuwa tayari
kuhudumia jamii na wenye hamu ya kufanya kazi na watu wengine
Comments