MOURINHO SASA HURU KUREJEA CHELSEA BAADA YA KUFUKUZWA 'KISTAARABU' REAL MADRID
IMEWEKWA MEI 21, 2013 SAA 12:30 ASUBUHI
KAMA
amefukuzwa. Kocha Jose Mourinho yuko huru kurejea Chelsea, baada ya
rais wa Real Madrid, Florentino Perez juzi usiku kusitisha malipo Pauni
12 za kuvunja mkataba wake.
Perez
ametangaza kwamba, matatizo ya Mourinho miaka yake mitatu kazini
Bernabeu vitaisha mwezi ujao, baada ya kufanya mazungumzo na kocha huyo
Mreno mwishoni mwa wiki.
Mourinho
ana miaka minne katika mkataba wake bado. Ataiongoza timu Jumapili
dhidi ya Real Sociedad na kisha katika mechi ya nyumbani dhidi ya
Osasuna, Juni 1.
Special anaondoka: Jose Mourinho amefukuzwa ukocha wa Real Madrid na sasa yuko kurejea Chelsea
Kitimutimu: Mourinho alitolewa nje kwa kadi nyekundu Real ikilala 2-1 katika Fainali ya Copa Del Rey dhidi ya Atletico
Perez,
mwenye matumaini ya kumtwaa kocha wa Paris Saint-Germain, Carlo
Ancelotti, alisema: "Klabu na kocha tumekubaliana ni wakati mwafaka
kumaliza uhusiano wetu. Tungependa kumshukuru Jose kwa kazi yote ngumu.
Timu imeimarika katika miaka yake mitatu na tunamtakia kila la heri.’
Special
One ataondoka rasmi katika nafasi yake Bernabeu Juni 3 na Chelsea
inatumai kumtambulisha katika Mkutano na Waandishi wa Habari Stamford
Bridge wiki inayofuata.
Anachukua nafasi: Kocha wa PSG, Carlo Ancelotti anatarajiwa kuvaa viatu vya Mourinho
Njoo nyumbani: Kurejea kwa Mourinho Chelsea kutakuwa jambo kubwa na zuri mbele ya umati wa Stamford Bridge
REKODI: Mourinho ana rekodi nzuri zaidi ya ushindi katika Ligi Kuu England kihistoria
Comments