NMB YASHIRIKI MAONYESHO YA BIASHARA TANGA
Waziri
wa Viwanda na Biashara Mhe. Abdallah Kigoda akipewa maelezo juu ya
huduma na bidhaa zinazotolewa na benki ya NMB kutoka kwa Meneja wa NMB
Tawi la Madaraka, Juma Mpimbi alipotembelea banda la NMB wakati wa
ufunguzi wa maonyesho ya biashara mkoani Tanga.
Waziri
wa Viwanda na Biashara Mhe. Abdallah Kigoda akisalimiana na Ofisa wa
benki ya NMB tawi la Madaraka, Elvis Shao alipotembelea banda la NMB
wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya biashara mkoani Tanga. Wakishuhudia
ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Chiku Gallawa (pili kulia) na Meneja wa
NMB Tawi la Madaraka, Juma Mpimbi
Maofisa
wa benki ya NMB Tawi la Madaraka wakiwa katika banda la NMB wakati wa
ufunguzi wa maonyesho ya biashara yaliyozinduliwa na Waziri wa Viwanda
na Biashara Mhe. Abdallah Kigoda mkoani Tanga.
Comments