ANKAL AISHUKURU HOSPITALI YA KILUTHERI YA HAYDOM KWA KUMHUDUMIA VYEMA MWANAE
Nachukua
nafasi hii kutoa shukurani zangu za dhati kutoka katika kilindi cha
moyo wangu kwa Hospitali ya Kilutheri ya Hydom iliyoko mkoani Manyara
kwa matibabu waliyompatia mwanangu Ally Hassan (16) aliyelazwa
hospitalini hapo tokea siku ya Alhamisi Juni 13, 2013 akiwa hajitambui
(in a coma) kwa muda wa siku nne mfululizo baada kuugua malaria sugu.
Shukurani
maalum ziwaendee madaktari na wauguzi wote wa wodi ya wagonjwa mahututi
(ICU) ambao kwa siku hizo nne tulikesha nao kumuuguza Ally ambaye
aliletwa hapo toka Katesh alikoenda kumtembelea mama yake wakati huu wa
likizo akiwa hana fahamu. Kwa upendo, weledi na utaalamu wenu hatimaye
mlifaniklwa kupambana na malaria hiyo kwa ukamilifu. Hivi sasa Ally
hajambo na anaendelea kupata nafuu kila dakika.
Mama mzazi, Baba mlezi, mjomba, shangazi, mamdogo na mamkubwa mliojitoa kumsaidia Ally nawashukuru sana sana kwa upendo wenu.
AHSANTENI SANA SANA SANA.
Madaktari
na wauguzi wa Hospitali ya Kilutheri ya Haydom sina cha kuwalipa zaidi
ya kutoa ahsante kwa wote mliomshughulikia Ally pamoja na wagonjwa
wengine waliolazwa hapo (nilishuhudia kwa macho yangu jinsi mlivyokuwa
mkiwashughulikia wagonjwa wote kwa upendo na weledi kila dakika
walipohitaji uangalizi) na kupata nafuu.
Kwa
niaba ya wagonjwa wengine waliopata huduma na kupata nafuu, natoa pia
ahsante kwa kazi njema, ya weledi na upendo mnaoonesha kwa kila mgonjwa
anayefika kutibiwa hapo Hydom. Ninyi ni mfano wa kuigwa katika
mahospitali yetu yote hapa nchini.
NAOMBA MOLA AWALIPE KWA KUWAZIDISHIA
PALE MLIPOPUNGUKIWA. MBARIKWE SANA.
AMEN
-Muhidin Issa Michuzi
Ankal akiwa Haydom na na baba mlezi wa Ally Hassan (kushoto) na mjomba
Sehemu ya mbele ya hospitali ya Kilutheri ya Haydom, Manyara
Baadhi ya wodi za Hospitali ya Kilutheri ya Haydom, Manyara
Ankal akikesha kumuuguza mwanae Ally Hassan hospitalini hapo
Ally Hassan akiwa kitandani pake akiangaliwa na mama, mamdogo, mjomba na shangazi.
Comments