HAYA NI MATUSI YA RAIS WA RWANDA PAUL KAGAME KWA TANZANIA
Na Mwandishi Wetu
MATUSI ya Rais wa Rwanda Paul Kagame kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete yamewagawa Watanzania.
Rais
Kagame alimtukana Rais Kiwete kwa kuita ushauri wake kwamba ni ushauri
wa kijinga kwa wanyarandwa, awali Rais Kikwete alizishauri nchi za
Rwanda na Congo DRC kukutana na kumaliza tofauti zao kwa njia ya amani.
Rais
Kikwete alitoa ushauri huo wakati wa mkutano wa kujadili amani na
mpango wa ulinzi nchini Congo DRC uliofanyika katika Makao Makuu ya AU
mjini Addis Ababa Ethiopia.
Katika
ushauri huo Rais Kikwete alisema kwamba ni vyema Rais Kagame akakaa
katika meza ya mazungumzo ya amani na Rais wa Congo DRC Joseph Kabila
ili kumaliza tofauti zao badala ya kutumia nguvu ya kijeshi.
“Nimekaa
kimya kwa kipindi kirefu na kwa jinsi nilivyoweza kwa sababu nilifikiri
kwamba mazungumzo ya kipuuzi yaliyozungumzwa na watu wajinga
yamemalizika "alisema Rais Kagame.
Katika hatua nyingine Rai Kagame alisema kwamba ushauri huo wa Rais Kikwete ni sawa na kuwachezea wanyarandwa mbele ya mataifa. Rais
Kagame aliyasema hayo katika sherehe ya kuhitimu mafunzo ya maofisa wa
jeshi wapatao 45 katika kituo cha mafunzo ya kijeshi siku ya Juma Tatu
nchini Rwanda.
Ingawa
haijajulikana mara moja kwamba baadhi ya watu walioandika maoni yao
katika mtandao wa Facebook ni watanzania ama baadhi yao si watanzania,
huku wakidai kwamba Rais Kagame yuko sahihi
Comments