SHEHA WA TOMONDO AANZA MATIBABU NCHINI CHINA.
Madaktari Bingwa wa Hospitali ya Miot Mjini
Chenai Nchini India leo wanaanza kumfanyia huduma za matibabu Sheha wa
shehia ya Tomondo Mohd Omar Said { Kidevu } baada
ya kukamilisha uchunguzi wa matatizo yake kufuatia kumwagiwa Tindi kali
karibu mwezi mmoja uliopita.
Sheha Kidevu
aliyefika Nchini humo Tarahe 21 na kufanyiwa vipimo vyote vilivyohusika anaanza matibabu kwa hatua ya kupandikizwa ngozi
katika sehemu zake alizoathirika kutokana na kuungua kwa maji ya Tindi
kali hiyo.
Akizungumza
kwa njia ya Simu Daktari aliyeambatana na Sheha
huyo Dr. Said Ali Said { Mkarafuu } alieleza kwamba Madaktari wa India
wameelezea kuridhishwa kwao na hatua kubwa iliyochukuliwa na Madaktari
wa Zanzibar ya kumpatia tiba sahihi mgonjwa huyo.
Dr. Said
alisema Madaktari hao Bingwa wa India wamekaririwa wakisema kwamba
wamepata matumaini ya huduma hizo alizofanyiwa Zanzibar ambazo zinawapa
hatua ya pili ya kuendelea na Tiba ya Sheha Kidevu.
“ Amefanyiwa uchunguzi wa vipimo vyote na kubainika kwamba jicho
lake Sheha Kidevu ambalo liliwahi kupata athari kidogo limewahiwa na
Madaktari wa Zanzibar wakiongozwa na Dr. Gang na
Dr. Slim na hivi sasa liko katika hali ya kawaida “. Alifafanua Dr. Said
Mkarafuu.
Alifahamisha
kwamba Madaktari hao wa Hospitali ya Miot Mjini Chenai Nchini India
wameelezea matarajio yao kwa mgonjwa huyo kuendelea na huduma za
matibabu kwa haraka licha ya Madaktari hao kutokutaja huduma hizo
zitamalizika katika kipindi gani.
Kabla Sheha
Mohd Kidevu alikuwa akipatiwa huduma za matibabu katika Hospitali Kuu ya
Mnazi Mmoja kwa takriban Mwezi Mmoja sasa kutokana na kuathirika sehemu ya kulia ya kifua chake, Bega pamoja na baadhi
ya maeneo ya mapaja.
Sheha huyo wa
Shehia ya Tomondo Mohd Omar Said Kidevu alipatwa na mtihani huo wa
kumwagiwa Tindi kali { Acid } na mtu
asiyejuilikana Usiku wa tarehe 22 Mei Mwaka huu wakati akienda kutafuta Maji mara baada ya kurejea kwenye Ibada ya sala ya
Ishaa.
Vitendo vya
matumizi mabaya ya tindikali vinavyofanywa na baadhi ya watu vinaonekana
kuanza kuwatia hofu wananchi na hasa baadhi ya Viongozi katika maeneo
mbali mbali hapa Zanzibar.
Comments