Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam jioni hii, kuhusu moja ya mafanikio ya ziara ya kikazi ya Rais Jakaya Kikwete, Uingereza ambapo ameahidiwa na Klabu ya Sunderland ya Uingereza na Symbion ya Marekani kujenga Kituo kikubwa cha maendeleo ya mchezo wa soka nchini (Soccer Academy). Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo wa wizara hiyo, Leonard Thadeo. (PICHA NA KAMANDSA RICHARD MWAIKENDA)
Baadhi ya wanahabari wakiwa kazini
Baadhi ya wanahabari wakiwa kazini
TAARIFA YA WAZIRI WA HABARI, VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO, DK. FENELLA MUKANGARA KWA
VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UJENZI WA ACADEMY YA MPIRA WA MIGUU HAPA NCHINI
§
Kama
mnavyofahamu, hivi karibuni Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania
alikuwa katika ziara yake ya kikazi nchini Uingereza.
§
Mhe.
Rais alipokuwa nchini Uingereza alitembelea Club ya Sunderland.
Mhe. Rais alihahidiwa kujengewa
Academy ya Mpira wa Miguu
na Kampuni ya Symbion Power ya Marekani ambayo itashirikiana na Club ya
Sanderland katika kuindesha.
§
Hiyo Academy tunategemea itawezesha
clubs zetu kupata wachezaji walio bora na walioandaliwa kuwa wachezaji wa taifa
na kimataifa na hivyo kuboresha timu yetu ya Taifa na kuendelea kukuza muamuko
wa masuala ya mpira wa miguu nchini.
§
Tunatarajia
suala hili litafanyika na kutekelezwa mapema iwezekanavyo
§
Katika mpango huo, Kampuni ya Symbion pia itajenga viwanja
vya michezo (sports courts) pale Kidongo Chekundu.
§
Kutokana na umuhimu wa suala
hili, viongozi wakuu wa Kampuni ya Symbion wanatarajia kuja hapa nchini na
nitakutana nao kwa ajili ya makubaliano mbalimbali na maandalizi ya
utekelezaji.
§
Hivi sasa kama Serikali
tunatafuta sehemu itakayojengwa Academy hiyo.
§
Matarajio au nia yetu ni
kujenga Academy hiyo Dar es Salaam au maeneo yaliyo karibu na Dar es Salaam.
§
Napenda nichukue fursa hii
kumshukuru sana Mh. Rais kwa kufanikisha suala hili.
§
Napenda pia kumshukuru Mbunge wa Ilala Mhe.
Mussa Zungu Azzan kwa kuwezesha kupatikana kwa viwanja vya Kidongo Chekundu.
§
Napenda pia kutumia fursa hii
kuwapongeza na kuwashukuru vijana wetu wa timu ya Taifa ”Taifa Stars” kwa
juhudi na mchezo mzuri waliouonyesha wakati wa mechi yao na Timu ya Taifa ya
Ivory Coast jumapili iliyopita. Tupo
pamoja nao na tutaendelea kuhakikisha tunawajengea uwezo zaidi ili waweze
kupata mafanikio makubwa huko mbeleni.
§
Huko tunakoelekea, Academy
itakuwa chimbuko la kupata wachezaji wazuri wa timu ya Taifa.
Asanteni kwa kunisikiliza
Comments