TAARIFA ZA MICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA KANDANDA TANZANIA TFF
MAKOCHA
STARS, IVORY COAST ANA KWA ANA
Wakati timu
ya Ivory Coast imewasili nchini jana usiku (Juni 13 mwaka huu) kwa ndege maalum,
kocha wa timu hiyo Sabri Lamouchi na mwenzake wa Taifa Stars, Kim Poulsen
watakutana na waandishi wa habari kuzungumzia mechi
yao.
Mkutano huo
utafanyika kesho (Juni 15 mwaka huu) saa 4 kamili asubuhi kwenye ofisi za
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Mkutano huo pia utajumuisha makocha
wa timu zote mbili. Ivory Coast inafanya mazoezi yake ya kwanza leo (Juni 14
mwaka huu) saa 9 alasiri kwenye viwanja vya Gymkhana.
Timu zote
kesho (Juni 15 mwaka huu) zitafanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Taifa,
Dar es Salaam. Ivory Coast watafanya mazoezi saa 9 kabla ya kuwapisha Stars saa
10 kamili. Maandalizi yanaendelea vizuri ikiwemo kuwasili kwa maofisa wote wa
mechi itakayochezwa Jumapili saa 9 kamili alasiri.
Wakati huo
huo, mauzo ya tiketi kwa ajili ya mechi hiyo yameanza leo mchana (Juni 14 mwaka
huu) katika vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo,
mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta
Buguruni, City Sports Lounge iliyoko Mtaa wa Samora na Azikiwe, Dar Live
Mbagala, BMM Salon iliyoko Sinza Madukani na Uwanja wa Taifa.
Mauzo
yataendelea kesho katika vituo hivyo, wakati siku ya mchezo yatafanyika Uwanja
wa Taifa. Viingilio katika mechi hiyo ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya
Afrika katika kundi C ni sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000 VIP C, sh.
20,000 VIP B na VIP A sh. 30,000. Pia kuna kadi maalumu 100 kwa viti vya Wageni
Maalumu (VVIP) zinazopatikana kwa sh. 50,000 katika ofisi za
TFF.
TFF YATOA
NOTISI YA MKUTANO MKUU
Rais wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ametoa notisi kwa
wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa Shirikisho utakaofanyika Julai 13 mwaka huu
kwenye ukumbi wa NSSF Waterfront jijini Dar es Salaam ukiwa na ajenda moja ya
marekebisho ya Katiba.
Notisi hiyo
imetolewa juzi (Juni 12 mwaka huu). Rais ameitisha Mkutano huo kwa mujibu wa
Ibara ya 25(1) ya Katiba ya TFF baada ya kupata maagizo kutoka Shirikisho la
Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kwa barua yake ya Aprili 29 mwaka
huu.
Ajenda rasmi
na taarifa nyingine zitatumwa kwa wajumbe siku 15 kabla ya Mkutano huo kwa
mujibu wa Ibara ya 25(4) ya Katiba ya TFF. Wanachama wa TFF ambao ni vyama vya
mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu wanatakiwa kutuma majina ya wajumbe
halali.
TFF inapenda
kuwakumbusha wanachama wake kutuma majina ya wajumbe halali ili kufanikisha
maandalizi ya Mkutano huo. Ni vizuri kuhakikisha kuwa jina linalotumwa ni la
mjumbe halali wa Mkutano Mkuu kwa mujibu wa Katiba ya
TFF.
RCL YAINGIA
HATUA YA TATU WIKIENDI HII
Mechi za
kwanza za hatua ya tatu ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kuwania nafasi tatu
za kupanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao zinachezwa wikiendi hii kwenye
viwanja vinne tofauti.
Mechi za
kesho (Jumamosi) ni kati ya Kariakoo ya Lindi na Friends Rangers ya Dar es
Salaam utakaochezwa katika Uwanja wa Ilulu mjini Lindi wakati Uwanja wa
Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya wenyeji
Kimondo SC na Njombe Mji.
Timu za
Machava FC ya Kilimanjaro na Stand United FC ya Shinyanga, Polisi Jamii ya Mara
na Katavi Warriors ya Katavi zilizokuwa zipambane kesho mechi zao zimesogezwa
mbele hadi keshokutwa (Jumapili). Mechi hizo zimesogezwa kutokana na viwanja vya
Ushirika mjini Moshi na Karume mjini Musoma kuwa na shughuli nyingine za
kijamii.
Hata hivyo,
TFF imesisitiza kuwa ikibainika kuwa viwanja hivyo havikutumika kwa shughuli za
kijamii siku hiyo ya Jumamosi, hatua kali zitachukuliwa kwa wanachama wake
(vyama vya mpira wa miguu vya mikoa husika).
Mechi za
marudiano za hatua hiyo ya tatu zitachezwa Juni 19 mwaka huu. Hatua ya nne ya
RCL itachezwa kati ya Juni 23 na 23 mwaka huu wakati mechi za marudiano
zitachezwa kati ya Juni 29 na 30 mwaka huu.
RAMBIRAMBI
MSIBA WA ABDALLAH MSAMBA
Shrikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha
mchezaji wa zamani wa timu za Pan Africans, Simba na Taifa Stars, Abdallah
Msamba kilichotokea juzi usiku (Juni 12 mwaka huu) jijini Dar es
Salaam.
Msiba huo ni
mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Msamba akiwa
mchezaji, na baadaye kocha wa timu kadhaa alitoa mchango mkubwa kwa timu
mbalimbali alizochezea na kufundisha ikiwemo Villa Squad, hivyo mchango wake
tutaukumbuka daima.
TFF inatoa
pole kwa familia ya marehemu Msamba, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es
Salaam (DRFA), Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kinondoni (KIFA) na klabu ya
Villa Squad na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu
cha msiba huo mzito.
Maziko ya
mchezaji huyo yamefanyika leo (Juni 14 mwaka huu) katika makaburi ya Ndugumbi
mkoani Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji wakiwemo wachezaji
wa zamani na viongozi mpira wa miguu nchini. Mungu aiweke roho ya marehemu
Msamba mahali pema peponi. Amina
Comments