Ziara ya Rais Obama yazidi kuwatia kiwewe wasomi
Dar es Salaam. Ziara ya Rais wa Marekani, Barack Obama bado imeendelea kuwatia kiwewe Watanzania wakiwamo wasomi na wanasiasa.
Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Profesa Ibrahim
Lipumba jana alisisitiza kwamba Rais huyo anakuja nchini kuchunguza
masuala ya madini hususan urani.
Lakini nao wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
(UDSM), wamepata hofu wakisema wana wasiwasi Tanzania itakachofaidika
kwa ziara hiyo. Wakizungumza jana kwa nyakati tofauti, Mhadhiri wa
Kitengo cha Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala wa Umma, Sabatto
Nyamsenda alisema hofu kubwa iliyopo inatokana na ubovu wa sera za
Serikali katika masuala ya uwekezaji.
Nyamsenda aliongeza kuwa viongozi wa Serikali
wamesharidhia uporaji wa rasilimali zake kupitia sera na mikataba mibovu
isiyomnufaisha Mtanzania.
Profesa Robert Mabele kutoka kitengo cha uchumi
chuoni hapo alisema pamoja na uhusiano ambayo Rais Kikwete amejitahidi
kuujenga miongoni mwa nchi kubwa duniani, lakini hatuwezi kufaidika
endapo hatutakuwa na sera nzuri za uwekezaji.
Dk Jehovaness Aikaeli wa kitengo cha uchumi chuoni hapo alisema ujio wa rais huyo hautaweza kuleta mabadiliko yoyote kama inavyodhaniwa na Watanzania wengi.
Dk Jehovaness Aikaeli wa kitengo cha uchumi chuoni hapo alisema ujio wa rais huyo hautaweza kuleta mabadiliko yoyote kama inavyodhaniwa na Watanzania wengi.
Maoni hayo yanatolewa wakati juzi Balozi wa
Marekani nchini, Alfonso Lenhardt alitaja sababu za Obama kuja Tanzania
kwamba ni kutokana na sifa nzuri za Tanzania. Sifa hizo zilizomvuta
Rais Obama ni utawala bora, demokrasia na mazingira bora ya uwekezaji
yanayosabisha kukua kwa uchumi.
Balozi wa Marekani alisema Tanzania ni nchi ya
mfano linapokuja suala la uongozi bora na ndiyo maana imekuwa na amani,
utulivu kwa muda mrefu ikilinganishwa na nchi nyingi za Kusini mwa
Jangwa la Sahara.
‘‘Rais Obama anakuja kuunga mkono juhudi za
Watanzania katika kutengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji na pia
amevutiwa na ukuaji wa uchumi,’’ alisema Lenhardt.
Comments