Dk. Slaa, Dk. Kikwete; Nani atakayetuvingirishia jiwe la Rushwa na Ufisadi?
BAADA
ya Kifo cha Muasisi na Mpigania wa Uhuru wa Taifa hili Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere, kama ilivyokuwa wakati wa Kifo cha Yesu Kristo,
yaliyotokea haya!
“Hata
sabato ilipokwisha kupita, Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yakobo,
na Salome walinunua manukato wapate kwenda kumpaka. Hata alfajiri
mapema, siku ya kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza
kuchomoza;
Wakasemezana wao kwa wao, Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe
mlangoni pa kaburi? Hata walipotazama, waliona ya kuwa lile jiwe
limekwisha kuvingirishwa; nalo lilikuwa kubwa mno.
Wakaingia kaburini wakaona kijana ameketi upande wa kuume, amevaa vazi jeupe; wakastaajabu”. Marko 16:3-5
Toka
mwenye uchungu na nchi hii (Nyerere) aondoke, nchi iliingia
kugandamizwa na jiwe kubwa la uuzwaji wa viwanda, Biashara huria,
uwekezaji uchwara, madawa ya kulevya, mauaji yaliyokithiri, Rushwa na
Ufisaji Mkubwa; tunajiuliza, ni ani atakayetuvingilishia Jiwe hilo?
Biblia
inasema, “Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome
walinunua manukato wapate kwenda kumpaka. Hata alfajiri mapema, siku ya
kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza”
Mbona
sisi siku za uchaguzi kwenye sanduku la kura alfajiri, tunapiga kura za
kukumbatia na kustawisha Rushwa, Madawa ya Kulevya yanayoathiri na kuua
watoto, wizi na utoroshaji wa Rasilimali zetu, Madawa na bidhaa feki,
na hatimae Ufisadi uliokubuhu viendelee?.
Wale
akina mama wanne, walisemezana wao kwa wao na kumtafuta nani
atakayewaondolee lile jiwe mlangoni ili waone maisha Bora kwa kila mtu
yaliyokuwa yakipatikana kwa kumuona Yesu, japo alikuwa kaburini alikuwa
na nguvu na uwezo huo.
Leo
hii, Taasisi na Asasi za Dini, Wanaharakati, Vyombo vya Haki za
binadamu, Wanasheria, Wanasiasa, Wabunge, Viongozi wa Serikali, Vyama
vya Siasa na Mtanzania mmoja mmoja wenye uchungu na nchi hii wakiwemo
Wana habari, mnasemezana nini?
Bibilia
katika kitabu cha pili cha Wafalme 13:20 inasema, “Elisha akafa, nao
wakamzika. Basi vikosi vya Wamoabi wakaingia katika nchi mwanzo wa
mwaka.
“Ikawa,
walipokuwa wakimzika mtu, angalia, waliona kikosi; wakamtupa yule mtu
kaburini mwa Elisha; mara yule maiti alipoigusa mifupa ya Elisha,
alifufuka, akasimama kwa miguu.
Naamini
Tanzania wapo watu wenye mifupa yaani Roho, Elimu, Ujuzi, Hekima,
Maadili, Uchungu, Upendo na Ueledi wa Usia na Chembechembe za Nyerere na
Edward Moringe Sokoine, wanaoweza kuifufua nchi kama ilivyofanya mifupa
ya Elisha kwa ile maiti.
Ili
kuondokana na Jiwe kubwa la Rushwa, Ufisadi, Kodi za Simu, Madawa ya
kulevya, Dhuluma, Mauaji, Maisha magumu kwa kila sekta (Wafanyakazi wa
taasisi binafsi na za Umma, Walimu waliokata tamaa, Wakulima, Wafugaji
na wengine;
Dawa
na Mfupa wa kwanza utakaofufua matumaini mapya ya Taifa letu, ni kwenye
sanduku la kura 2014 kwenye chaguzi za Serikali za Mitaa, na 2015
kwenye Uchaguzi Mkuu kwa wale ambao Mungu atakaowachagua kuuona mwaka!
Narudia, Suluhisho ni Sanduku la Kura.
Lakini
Dawa na Mfupa wa pili ni taasisi za Haki za binadamu, Wanaharakati,
Vyombo vya Sheria, na mtu mmoja mmoja katika eneo hilo, waumizwa na hali
hii, wasimame pamoja ili kulikomboa Taifa hili kwenye ukoloni huu
mkongwe wa pili.
Tumeshudia
watuhumiwa wa madawa ya kulevya Wanakamatwa; lakini wakihukumiwa
wanakata rufaa, na huko kwenye rufaa ndiko rushwa na ufisadi unatembea,
siku mbili wanaachiwa unawaona mitaani, na watoto wetu wanaendelea
kuumia na hatimae wanakufa.
Tumemsikia
Rais Jakaya Kikwete akiwaamuru wakimbizi na Wageni waliojipenyeza
nchini bila utaratibu maalum, warudi makwao! Na kwamba wasipofanya
hivyo! Watasakwa na kurudishwa kwa nguvu. Ni wangapi wamejificha nchini?
Nani anawajua? Hakuba.
Lini
watanzania sasa, tutatumia sanduku la kura kama Malaika wa kutuondolea
jiwe, kurudisha heshima yetu kwa kuwaondoa wageni wanaopora Rasilimali
zetu kwa uwekezaji uchwara unaoitwa mikataba ya siri?
Siri gani zinazofanywa ndani ya nchi yetu sisi tukiwemo? Biblia inasema Siri zote ni za Mingu.
“Mambo
ya siri ni ya Bwana, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu
sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria
hii.“Kumbukumbumu la Torati 29:29.
nyeregete@yahoo.co.uk 0715-933308
Comments