MWENYEKITI WA WILAYA RORYA WA CHADEMA AMBAYE PIA NI DIWANI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA UZINZI NA MKE WA MTU
RORYA,Tanzania
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya
Rorya mkoani Mara ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Tai kupitia Chama
hicho, Masirori Kyorang amefikishwa Katika Mahakama ya Mwanzo Shirati
kujibu mashitaka ya ugoni.
Kwa mujibu wa kesi hiyo, Kyorang anadaiwa kushikwa ugoni na mke wa
mlinzi wa Mbunge wa Jimbo la Rorya wakiwa gesti ya Triple Kabwana katika
mji mdogo wa Shirati, suiku wa kuamkia jana.
Akisomewa Mashitaka hayo jana Julai 24, na Mwendesha Mashitaka wa
Polisi mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Shirati Dock Nyatega ,
ambapo ilidaiwa kuwa mheshimiwa Masirori alikamatwa mida ya saa 3
usiku, katika chumbani akiwa na mke wa mlinzi huyo wa Mbunge wa Jimbo la
Rorya aliyejulikana kwa jina Pendo Omolo.
Mtuhumiwa Masirori alikana Mashitaka
yake na kupata Dhamana hadi kesi yake itakapotajwa tena Julai 29 ,
ambapo Mke huyo Pendo amekwenda Nyumbanio kwao hadi Shauri hilo
litakapoanza kusikilizwa na kubaini Ukweli wake baada ya Ushahidi
kutolewa Mahakamani alisikika akisema Hakimu Nyatega zaidi soma hapa http://www.bashir-nkoromo.blogspot.com/
Comments