Rais Jakaya Kikwete (kushoto) akisalimiana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda huku Makamu wa Rais Dk. Mohamed Ghalib Bilali akiangalia wakati alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo, akitokea Marekani katika ziara ya kikazi. (PICHA NA IKULU)
THE UNITED REPUBLIC
OF TANZANIA
DIRECTORATE OF
PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
Fax: 255-22-2113425 |
PRESIDENT’S OFFICE,
THE
STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
Kikwete arejea nyumbani kutoka Canada na Marekani
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amerejea nchini mchana wa leo, Jumatatu,
Septemba , 2013, baada ya ziara ya kikazi yenye mafanikio makubwa katika
Marekani na Canada.
Miongoni
mwa shughuli nyingine nyingi katika ziara hiyo, Rais Kikwete alihutubia Kikao
cha 68 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN)
mjini New York.
Rais
Kikwete ambaye aliondoka nchini Jumapili ya Septemba 15 alianzia safari yake
mjini San Francisco, Marekani, ambako miongoni
mwa mambo mengine alizindua Ubalozi Mdogo wa Tanzania
katika Jimbo la California.
Rais
pia alikutana na kuzungumza na Jumuia ya Watanzania katika Jimbo hilo na kukaribishwa katika Jiji la Vallejo
katika sherehe za miaka 20 za uhusiano wa kimji kati ya Jiji hilo na mji wa Bagamoyo.
Ziara
ya Rais Kikwete San Francisco ilifuatiwa na ziara ya mjini Washington ambako shughuli zake kubwa zilikuwa
kukutana na viongozi wa Bunge la Marekani na pia kuhudhuria Hafla ya Chakula
cha Usiku cha Taasisi ya Kulinda Hifadhi na Mazingira ya Bunge la Marekani (ICCF) ambako alitunukiwa tuzo maalum za
Mtunzaji Mazingira Bora wa Mwaka.
Aidha,
Rais Kikwete alishuhudia utiaji wa saini mikataba ya kufungua Ofisi Ndogo za
Ubalozi wa Tanzania
katika majimbo mbali mbali ya Marekani.
Baada
ya hapo, Rais Kikwete alikwenda Canada
ambako alitunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Udaktari wa Sheria na Chuo maarufu na
kikongwe cha Canada cha Guelph ambacho ni maarufu
duniani kwa shughuli na utafiti wa kilimo.
Kufuatia
ziara hiyo ya Canada, Rais Kikwete alikwenda New York ambako alikuwa na shughuli
nyingi ikiwa ni pamoja na kuhutubia Kikao cha 68 cha Baraza Kuu la UN Ijumaa ya wiki iliyopita, akakutana
na Katibu Mkuu wa UN Mheshimiwa Ban
Ki Moon, akashiriki kikao maalum cha wakuu wa nchi kujadili hali ya Mashariki
mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC)
kilichoitishwa na Mheshimiwa Ban Ki Moon.
Akiwa
mjini New York,
Rais Kikwete pia alikuwa kiongozi pekee wa Afrika aliyealikwa kushiriki katika
Mkutano wa Rais wa Marekani Mheshimiwa Barack Obama na taasisi zisizokuwa za
kiserikali duniani na pia alihudhuria Halfa Maalum iliyoandaliwa na Rais Obama
alipomaliza kuhutubia Kikao cha 68 cha Baraza Kuu la UN.
Aidha,
Rais Kikwete alishiriki Mkutano wa Mwaka wa Taasisi ya Clinton Global Initiative na pia akawa mzungumzaji rasmi katika
Mkutano wa Kupambana na Ujangili Duniani uliotishwa na Rais Ali Omar Bongo
Ondemba wa Gabon.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
30 Septemba, 2013
Comments