Amis Tambwe wa Simba akiudhibiti mpira huku akizongwa na Ernest Mwalupani wa Kagera Sugar wakati timu hizo zilipopambana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom, Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Hata hivyo baada ya Kagera kusawazisha kwa njia ya penati katika dakika ya 89, vurugu zilizuka ambapo mashabiki wa Simba walianza kuvunja viti na kuanza kurusha viti wakiulaumu uamuzi mbaya wa waamuzi.
Baada ya kuona hivyo FFU waliamua kuwafurumusha kwa kupiga mabomu ya machozi uwanjani hapo.
Baada ya kuona hivyo FFU waliamua kuwafurumusha kwa kupiga mabomu ya machozi uwanjani hapo.
Comments