Mtaalamu kutoka TASAF Makao makuu Bi. Mercy Mandawa mwenye miwani na kompyuta mpakato akiandika baadhi ya mambo yaliyojitokeza
kwenye mafunzo ya wawezeshaji ngazi ya wilaya mjini Dodoma.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya namna ya kuendesha kazi
yautambuzi wa kaya masikini ngazi ya halmashauri ya wilaya wakimsikiliza mtoa
mada hayupo pichani katika ukumbi wa shule ya sekondari ya Dodoma.
Mtoa mada katika mafunzo ya wawezeshaji ngazi ya Wilaya, Bw.
Andrew Kibona akitoa mada kwenye mafunmzo hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa
shule ya sekondari ya Dodoma.
Washiriki wa mafunzo ya uwezeshaji wa mpango wa kunusuru
kaya masikini katika manispaa ya Dodoma wakimsikiliza mtoa mada hayupo pichani
juu ya namna ya kuzitambua kaya masikini .
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii,TASAF uimeanza utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya masikini katika mikoa ya
Dodoma, Singida ,Kigoma na Katavi ambako mafunzo kwa wawezeshaji wa Mpango huo
ngazi ya halmashauri za wilaya yameanza kutolewa.
Mpango huo utakaotekelezwa nchini kote kwa awamu, tayari
umekamilika katika mikoa ya Lindi na Mtwara ambako kaya masikini zitaanza
kupatiwa ruzuku kwa ajili ya kuboresha afya kwa mama wajawazito na watoto
wenyer umnri wa chini ya miaka 5, na
kuziwezesha kaya husika kumudu gharama za elimu na matibabu kwa familia husika
ili kuboresha maisha yao.
Ruzuku hiyo ya fedha pia
inakusudiwa kuzijengea uwezo kaya masikini ziweze kuinua kipato kwa kuanzisha shughuli za kiuchumi kulingana
na mazingira ya eneo husika ili hatiomaye ziweze kuondokana na umasikini wa
kipato.
Akizungumza katika mkutano wa wawezeshaji ngazi ya
taifa mjini Dodoma, Bi Mercy Mandao
amehimiza umuhimu wa kuendesha zoezi zima la utanmbuzi wa kaya masikini kwa
uangalifu mkubwa ili hatimaye walengwa waweze kupatikana na kuondoa uwezekano
wa kuwaacha walengwa kutokana na kutozingatia vigezo maalumu ambavyo huwekwa na
wananchi wenyewe kwenye maeneo yao.
Zifiatazo ni picha za baadhi ya washiriki wa mafunzo ya wawezeshaji katika manispaa ya Dodoma yaliyoanza leo Jumanne . Mafunzo kaya hao yatolewa pia katika halmashauri zote za mikoa ya Singida, Kigoma, Katavi, Rukwa ,na Dodoma
Comments