Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza mwanafunzi wa kidato cha nne
Neema Steven Mtwanga(16) anayesoma katika shule ya sekondari Naboti
Makambako,Njombe baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika utunzi wa
insha katika shindano lililoandaliwa na Jumuiya ya uchumi ya maendeleo
kusini mwa Afrika(SADC).
Rais
Kikwete alimpongeza mwanafunzi huyo wakati wa hafla ya ufunguzi wa
mkutano wa 34 wa wakuu wa nchi za SADC unaofanyika katika mji wa kitalii
wa Victoria Falls, nchini Zimbabwe ambapo mwanafunzi huyo aliandika
insha inayohusu mabadiliko ya tabia nchi.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wakuu
na wawakilishi wa nchi za Jumuiya ya uchumi kusini mwa Afrika SADC muda
mfupi baada ya ufunguzi wa mkutano wa 34 wa jumuiya hiyo uliofanyika
katika hoteli ya Elephant Hills mjini Victoria Falls Zimbabwe
leo.Katikati ji mwenyeji wa Mkutano huo Rais Robert Mugabe na mkewe
Grace Mugabe
Wanafunzi wa shule hiyo.
---
Γ Ni Neema Steven kutoka Shule ya Sekondari ya Naboti, Njombe
Γ Awabwaga washindani 39 wa kanda mbali na wa nyumbani
Mtoto wa
Kitanzania,msichana Neema Steven Mtwanga, ameibuka kinara katika Mashindano ya
Utunzi wa Insha katika nchi wanachama wa Jumuia ya Maendeleo ya Kusini mwa
Afrika (SADC) kwa kushika nafasi ya kwanza miongoni mwa washindani 39
waliowania Tuzo ya Utunzi wa Insha hiyo kwa Mwaka 2014.
Msichana Neema Steven
Mtwanga, 16, kutoka Shule ya Sekondari ya Naboti, Mkoa wa Njombe, ametunukiwa
Tuzo ya ushindi huo katika Mkutano wa 34 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama
wa SADC ulioanza leo katika Hoteli ya Elephant Hills Resort, Victoria Falls,
Zimbabwe.
Nafasi ya pili imeshikwa
na Kudzai Ncube kutoka Shule ya Sekondari ya Mazowe nchini Zimbabwe na nafasi
ya tatu imeshikwa na Manxoba Msibi kutoka Shule ya Sekondari ya Etjendlovu
katika Swaziland.
Kwa ushindi huo, Neema
Steven Mtwanga ambaye yuko kidato cha nne, amezawadiwa hundi ya dola za
Marekani 1500 ambayo ni sawa na shilingi
milioni 2.3 na amelipiwa gharama zote za
kumwezesha kushiriki katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za SADC na kukabidhiwa
zawadi hiyo. Aidha, Neema amepewa zawadi ya ipad kwa ajili ya matumizi yake ya
teknolojia ya mawasiliano na habari.
Mashindano hayo ya Insha
ya Mwaka 2014 yalianzishwa rasmi Oktoba,
2013 ambako washindani walitakiwa kuandika Insha kuhusu mada: “Climate
Change is having adverse effect on the socio-economic development in the
Region. What should the Education Sector do to mitigate the impact on the youth”
– Mabadiliko ya Tabia Nchi yanaathiri maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Kanda ya SADC. Nini Sekta ya Elimu ifanye
kupunguza athari hizo kwa vijana?
Insha 39 zilipokelewa
kutoka nchi 13 kati ya nchi 15 wanachama wa SADC ikiwa ni Insha tatu kwa kila
nchi. Insha zilipokelewa kutoka Tanzania, Angola, Botswana, Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo (DRC), Lesotho, Malawi, Mauritius, Mozambique, Namibia,
Afrika Kusini, Swaziland, Zambia na Zimbabwe.
Majaji wa kupitia na
kuamua washindi wa Insha hizo walitoka Tanzania, Zambia na Zimbabwe na
walikutana mjini Gaborone, Botswana, Julai, mwaka huu kupitia Insha zote na
kutoa uamuzi wa nani washindi.
Ujumbe wa Tanzania
kwenye Mkutano huo wa SADC umepokea kwa furaha ushindi wa msichana Neema
ukieleza kuwa ushindi huo umeiletea Tanzania heshima kubwa katika eneo la SADC
na nje ya eneo hilo.
Mwisho!
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
17 Agosti,2014
Comments