Rais Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Rais wa Zambia Michael Sata aliyefariki mwaka jana katika eneo la maziko ya viongozi wa kitaifa jijini Lusaka Zambia leo.Rais Kikwete alitumia wasaa huo pia kuweka shada la maua katika makaburi ya marais wa Zambia waliofariki Marehemu Frederick Chiluba na Levy Mwanawasa.(PICHA NA FREDDY MARO)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amekwenda
Saudi Arabia asubuhi ya leo, Jumapili, Januari 25, 2015, kuhani kifo cha Mfalme
Abdullah bin Abdul Aziz al Saud aliyefariki Alhamisi na kuzikwa Ijumaa ya wiki
iliyopita.
Baada
ya kuhani msiba wa Mfalme Abdullah, Rais Kikwete ataendelea na safari yake kwenda
nchi za Ujerumani na Ufaransa kwa ziara za kikazi.
Mjini
Berlin, Ujerumani ambako Rais Kikwete alitarajiwa kuwasili kesho, Jumatatu,
Januari 26, 2015, akitokea Riyadh, Saudi Arabia, anatarajiwa kuhudhuria Mkutano
wa Kimataifa wa Global Alliance for
Vaccines and Immunization (Gavi Alliance) ambako viongozi mbali mbali
duniani watajadili jinsi ya kuboresha mipango ya utoaji chanjo kwa watoto
wadogo hasa katika nchi zinazoendelea.
Baada
ya kumaliza ziara yake Ujerumani, Rais Kikwete atakwenda Ufaransa ambako
miongoni mwa mambo mengine atakutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa
Ufaransa.
Aidha,
Rais Kikwete atafungua jengo jipya la Ubalozi wa Tanzania katika Ufaransa na
pia nyumba ya balozi.
Rais
Kikwete baada ya kumaliza ziara zake za kikazi katika Ujerumani na Ufaransa
atakwenda Addis Ababa, Ethiopia, kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama
wa Umoja wa Afrika (AU).
Imetolewa
na:
Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM.
25 Januari, 2015
Comments