BOTSWANA YAITOA BAFANA BAFANA COSAFA, NAMIBIA YAWAVUA UBINGWA ZAMBIA

Wachezaji wa Botswana (jezi ya bluu) na Afrika Kusini (jezi ya njano) wakiwania mpira juu Jumapili
TIMU za Namibia na Botswana zimefanikiwa kutinga Nusu Fainali ya michuano ya Kombe la COSAFA 2015 baada ya ushindi wa matuta Jumapili Uwanja wa Moruleng mjini Rusternburg, Afrika Kusini.
Namibia imewatoa mabingwa watetezi Zambia kwa penalti 5-4 baada ya sare ya 0-0, wakati Botswana imewatoa wenyeji Afrika Kusini kwa penalti 7-6 baada ya sare ya bila mabao pia.
Afrika Kusini na Zambia sasa wanaangukia kwenye Nusu Fainali za vibonde, maarufu kama michuano ya Plate na wataungana na timu zitakazofungwa Jumatatu.
Robo Fainali za michuano hiyo zitaendelea Jumatatu kwa Ghana kumenyana na vinara wa Kundi B, Madagascar Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace Saa 11: 00 jioni.
Robo Fainali ya mwisho itafuatia kwa mchezo kati ya Msumbiji na Malawi Uwanja huo huo, Royal Bafokeng Sports Palace Saa 1:30 usiku.
Mchezaji wa Zambia (kijani) akipiga mpira mbele ya mchezaji wa namibia (nyekundu) 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.