Ingawa watu waliidharau Juventus, lakini imeanza mechi yake ya kwanza ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuwatuliza Real Madrid kwa kuwachapa 2-1.

Madrid ikiwa ugenini ilijikuta ikifungwa bao kupitia Alvaro Morata kabla ya Cristiano Ronaldo kuisawazishia Madrid.
Lakini shujaa wa Juventus alikuwa ni Carlos Tevez aliyefunga bao la pili katika kipindi cha pili kwa mkwaju wa penalti.
Madrid walijaribu kujitutumua lakini hawakuweza kusawazisha, hali inayowalazimu kuwa na kazi ngumu katika mechi ya marudiano kwao Santiago Benabeu.
Kesho Barcelona watakuwa na kazi ngumu dhidi ya Bayern Munich.









Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI