KOCHA Mfaransa, Patrick Liewig,
akizungumzia mikakati yake ya kiufundi baada ya kusaini mkataba wa
miaka miwili kuifundisha timu ya soka ya Stand United ya Shinyanga,
kwenye makao makuu ya kampuni ya Acacia jijini Dar es Salaam leo
Jumatatu Julai 20, 2015. Mkataba huo ni chini ya udhamini mnono wa
kampuni ya Acacia, inayomiliki migodi mitatu ya kuchimba dhahabu ya
Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara
Na K-VIS MEDIA
KLABU
ya soka ya Stand United ya mjini Shinyanga, imesaini mkataba wa miaka miwili na
kocha Mfaransa, Patrick Liewig, ili kuinoa timu hiyo itakayoshiriki ligi kuu
soka Tanzania bara msimu huu.
Akizungumza
wakati
wa kutiliana saini mkataba huo kwenye ofisi za wadhamini wakuu wa timu
hiyo, Acacia, jijini Dar es Salaam leo Julai 20, 2015, mwenyekiti wa
Stand
United, Amani Vincent alisema, baada ya kuangalia vigezo mbalimbali
ambavyo klabu hiyo ilihitaji, imeridhika pasina shaka kumuajiri kocha
huyo, ili ainoe timu yake kwa misimu miwili.
“Kocha
huyu
kama mjuavyo anayo sifa ya kuinua vipaji, na sisi tunataka kutengeneza
vipaji kutoka chini ili wachezaji hao waweze kuichezea timu yetu”,
amesema.Kocha
huyo aliwahi kuifundisha Simba ya Dar es Salaam, kwa miezi sita kabla ya
mkataba wake kusitishwa.Stand
United ambayo inashiriki ligi nkuu ya soka Tanzania bara kwa mara ya
pili, hivi karibuni ilipata udhamini mnono kutoka kampuni ya uchimbaji
madini, Acacia.
Akizungumza
kwenye hafla hiyo, Liewig, amesema, atahakikisha anajenga msingi mzuri timu
hiyo kwa kuwa na timu ya kikosi cha wachezaji chipukizi ili iwe na hazina ya
wachezaji. “Kinachohitajika ni kuwa na subira, kwani ninataka kujenga timu na
kazi hii siyo ya mara moja.”amesema.
Pamoja na mabo mengine, udhamini wa Acacia kwa timu hiyo ni pamoja na malipo ya kocha.
MWENYEKITI
wa Stand United ya Shinyanga, Amani Vincent, (wapili kulia),
akibadilishana hati za mkataba na Kocha Mfaransa, Patrick Liewig, makao
makuu ya kampuni ya Acacia, jijini Dar es Salaam leo Jumatatu Julai 20,
2015. Kulia ni Afisa Habari na Mawasiliano wa Acacia, Frederick Njoka
Liewig, (kushoto), na Amani Vincent, "wakimwaga" wino
Comments