Mkurugenzi
mtendaji wa kampuni ya Bushbucks Safaris iliyopo jijini Arusha Mustafa
Panju ambaye ni mmoja wa wagombea wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama
cha mapinduzi CCM akiongea katika mkutano wa hadhara katika kata mpya
ya Olmoti jana ambapo wagombea 12 walipata fursa ya kujitambulisha kwa
wananchi na kunadi sera zao,
Mustapha panju amesema kuwa kilicho msukuma kugombea nafasi hiyo ni
kuakikisha wananchi wa jimbo la arusha wanapata ridhaa ya kuwa na
maendeleo ya hali ya juu ikiwemo kuweza kukua kisayansi na kuweza
kufika mwezini.(Habari Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
Mustafa
Panju akiwa na wagombea wenzake wa chama hicho jana katika kata mpya ya
Olmoti jijini Arusha walipokwenda kujitambulisha kwa wananchi na kunadi
sera zao pia walipata fursa ya kutembelea kata ya Olasiti,Osunyai JR
Mtoto
aliyefika kusikiliza sera za wagombea Ubunge wa chama cha Mapinduzi
(CCM) akiwa ameshikilia kipeperushi cha mgombea Ubunge jimbo la Arusha
Mustafa Panju katika kata ya Osunyai JR
Comments