Nairobi:Kabla ya kuwasili kwa Obama



Rais Obama anatarajiwa wakati wowote kuanzia saa moja usiku
Biashara, usafiri na idadi ya watu mjini Nairobi imepungua kwa kiasi kikubwa saa chache kabla ya kuwasili kwa rais Obama
Abiria na madereva wanaotumia Bbararabara kuu jijini Nairobi wameathirika pakubwa na mipango kabambe za usalama zilizowekwa kwaajili ya ujio wa rais huyo wa Marekani.
Mabarabara yanayokaribiana na ile itakayotumika na Obama zimefungwa kwa umma.
Mabarabara yote atakayotumia Obama yamefungwa kwa umma
Na si hayo tu njia zote mkabala na zile zitakazotumika pia zimefungwa.
Obama anatarajiwa kutua nchini Kenya wakati wowote kutoka saa moja
Sekta ya matatu, njia kuu ya usafiri imelemazwa huku wahudumu wa magari ya abiria wakieleza kutokuwa na wateja.
Biashara ya bendera imenoga
Raia wengi wanaotumia barabara za Uhuru an Mombasa waliondoka mjini mapema huku wakihofia kuathirika na hatua ya kufungwa kwa barabara wanazotumia.
Maduka mengi ya kibiashara pia yalifungwa huku wafanyibiashara wakieleza kuandikisha idadi ndogo au hata kutoweko kwa wateja.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.