CHIKU ABWAO; UKAWA HAWANA NIA NZURI NA TAIFA HILI ,WATANZANIA KATAENI KUPELEKA IKULU WAFANYABIASHARA
Bi Chiku Abwao
Na MatukiodaimaBlog
ALIYEKUWA
mjumbe wa kamati kuu Taifa ya Chama cha Demokrasia na maendeleo
(CHADEMA) na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Bi Chiku Abwao
amevitaka vyombo vya habari nchini kusaidia kuwaokoa watanzania juu
ya kasi kubwa ya wafanyabiashara kung'ang'ania kwenda Ikulu kupitia
vyama vilivyokuwa vikiunda umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) kuwa
kinachoendelea ndani ya UKAWA ni hatari kwa ustawi wa Taifa na
sasa limekuwa ni genge la wafanyabiashara .
Ambwao
ambae alijiengua na Chadema hivi karibuni na kujiunga na chama cha ACT
Wazalendo alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wanahabari
mkoani Iringa juu ya maandalizi ya mkutano mkubwa wa ACT Wazalendo
utakaoongozwa na kiongozi mkuu wa ACT wazalendo Zitto Kabwe siku ya
jumapili wiki hii.
Alisema
pamoja na kuwa dhamila ya kukitoa chama cha mapinduzi ipo kupitia
vyama makini kama chama chake cha ACT Wazalendo ila bado kuna
njama mbaya zinazofanywa na vyama hivyo zilivyojipachika jina la
UKAWA kutokana na kuonyesha kwao wazi wazi kuwa wapo kimaslahi
zaidi na sio kwa ajili ya kulikomboa Taifa hili kwa kupinga
ufisadi ila wapo kwa ajili ya kusafisha na kutetea vitendo vya ufisadi
nchini jambo ambalo ni hatari na kuna kila sababu ya vyomba vya
habari nchini kusaidia kuelimisha jamii ili kukwepa kuingizwa
mkonge UKAWA wanaokumbatia ufisadi .
Alisema
kuwa yeye ni miongoni mwa wanasiasa wazuri hapa nchini ambae
kamwe hapendi siasa za maji taka za kukumbatia vitendo vya ufisadi
bali yupo kuona anakemea na kupinga kwa nguvu zote vitendo vya
ufisadi hapa nchini hivyo hakupendezwa kabisa na hatua ya CHADEMA
kumpokea waziri mkuu mstaafu Edward LOwasa kuwa mgombea urais huku
wakitambua wazi kuwa hana sifa ya kupinga ufisadi .
"Dhamira
ya kukitoa chama tawala madarakani ipo lakini kwa hatua ambayo
UKAWA wameonyesha ni kama wapo kwa ajili ya kushangilia vitendo
vya ufisadi kutokana na kukumbatia wale ambao awali waliwaita kuwa
ni mafisadi papa na leo wanatumia nguvu kubwa kuuaminisha umma kuwa
ni wasafi .......huu ni sawa na unafiki ambao UKAWA wameuonyesha na
kamwe itakuwa ni vigumu watanzania kuamini haya kwa leo ......huyu
akiwa CCM tulipaza sauti kuwa ni fisadi leo amekuja upinzani
tunauaminisha umma kuwa ni msafi .....hapana hii si siasa ya ukombozi
kwa mtanzania ila ni siasa ya kibiashara zaidi ambayo inafanyika
UKAWA....nawaombeni sana wanahabari nchini msaidie kuliokoa Taifa
hili mhakikishe kiongozi anayekwenda Ikulu awe mweye mwonekano wa
kuliokoa Taifa hili si wa kwenda kutumia kivuli cha Ikulu
kuboresha biashara zake " alisema Chiku
Bi
Chiku alisema Taifa hili kwa sasa limekwenda pabaya kwani
limekwisha tekwa na wafanyabiashara na kuwa kwa upande wake haamini
kama kweli kwa viongozi wa Chadema wanania nzuri na Taifa hili kwa
jinsi ambavyo wanavyotangulia pesa mbele na kutaka kuwaingiza kwa
nguvu kubwa wafanyabiashara Ikulu.
"
Hawa Chadema awali walikuwa mstari wa mbele kukemea ufisadi ila
leo wamegeuka na kukumbatia ufisadi na kuwa chama cha kuwasafisha
mafisadi kwa kumpa nafasi ya kuwa mgombea urais LOwasa na kumuacha
Dr Silaa ambae ni nembo ya siasa za Tanzania na nembo ya Chadema
.......Dr Slaa ni kiongozi msafi na muadilifu anayetambua kila
mmoja wetu na kuwa dhamira ya kutaka kuongoza nchi yawezekana
wanayo ila si dhamira nzuri kwa watanzania wanataka kutuuza
watanzania kwani tutakwenda pabaya kuliko hapa tulipo"
Hata
hivyo alisema kwa hali ya mambo yanavyokwenda ni wazi kuna wakati
mgumu zaidi kuliko wakati wote ule uliopita kwani ni mwaka huu
pekee ambao vyama vya upinzani vinakwenda katika uchaguzi mkuu kwa
lengo tofauti kabisa la kuwapeleka wafanyabiashara na wachafu Ikulu
tofauti na awali ambapo vyama vya upinzani kazi kubwa ilikuwa ni
kupinga CCM kwa ufisadi ila leo watanzania wanashuhudia upinzani
ukitetea ufisadi .
Bi
Chiku aliwataka wananchi kuwa makini na mbinu chafu ya UKAWA
kutaka kuliangamiza Taifa hili na kuchagua vyama makini na
viongozi makini kutoka chama cha ACT wazalendo ambacho ndicho chama
chenye sera na misingi imara ya kulikomboa Taifa hili kutoka
mikononi mwa CCM.
Kwani
alisema hata kinachotokea ndani ya UKAWA kwa sasa kwa viongozi
kujiuzulu nafasi zao ni sehemu ya pigo kutoka kwa mwenyezi Mungu kwa
kuona wale waliotumwa kuokoa wakikengeuka na kuwa waangamizaji
wakuu wa Taifa hili na kuwa hamshangi aliyekuwa mwenyekiti wa CUF
Prof Ibrahimu LIpumba na Dr Slaa kujiuzulu nafasi zao kwani kama
wangebaki ni wazi heshima yao ingeshuka zaidi ya hapo na kuwa ndani
ya UKAWA kuna viongozi wasiozidi wawili ambao wanafanya siasa kuwa
biashara binafsi .
Comments