BASATA YAWAPIGA MSASA VIONGOZI WA VYAMA VYA WASANII

 Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza (Kulia) akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya wasanii yaliyoandaliwa na Baraza hilo mapema wiki hii. Kulia kwake ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utamaduni anayeshughulikia Lugha kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Shani Kitoga
 Msanii mkongwe wa Sanaa za Maonesho Bw. Kassim Mbelemba maarufu kwa jina la Mzee Jangala akipokea cheti chake kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utamaduni anayeshughulikia Lugha kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Shani Kitoga baada ya kumaliza mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya wasanii yaliyoandaliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) mapema wiki hii.  
 Mwezeshaji wa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya Wasanii katika eneo la Hakimiliki na Hakishiriki Bw. John Kitime akipokea zawadi kutoka kwa mmoja wa viongozi wa vyama vya wasanii baada ya kutoa mafunzo kwa viongozi hao. 
Viongozi wa vyama vya Wasanii walioshiriki mafunzo ya Kujengewa Uwezo wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi Bi. Shani Kitoga
IMETOLEWA NA KITENDO CHA HABARI NA MAWASILIANO, BASATA.

BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limewapa mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo katika maeneo mbalimbali viongozi wa vyama na taasisi zinazojihusisha na wasanii ili kujenga ufanisi zaidi katika sekta ya Sanaa.

Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia Jumanne hadi Alhamisi ya wiki hii yalijikita katika kuwajengea uwezo Wasanii kwenye maeneo ya uandaaji bajeti, uandaaji wa mipango mikakati na sheria ya hakimiliki na hakishiriki na mikataba kwenye kazi za Sanaa. 

Akizungumza kwenye hafla ya kuyafunga mafunzo hayo, Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza alisema kwamba ana matumaini makubwa kwamba mafunzo haya kwa viongozi wa wasanii yataamsha ari katika utawala na utendaji wa sekta ya Sanaa na kufanikisha kupiga hatua kwa sekta hii muhimu.

“Nina imani katika mafunzo haya tutawaona viongozi wa wasanii mnakuwa na mipango ya muda mrefu, wa kati na mfupi maana hakuna jinsi tunaweza kuwaongoza wasanii bila kuwa na mipango” alisisitiza Mngereza.

Kuhusu suala la hakimiliki, hakishiriki na mikataba kwenye kazi za Sanaa  alisema kuwa ni tatizo linalowakumba wasanii wengi hivyo imani ya BASATA ni kuona viongozi hawa waliopatiwa mafunzo wanakuwa msaada kwa wasanii walio chini ya vyama vyao.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.