.Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), Michael
Mhondo akuzungumza na wadau mbalimbali (hawapo pichani) juu ya Mfuko
wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), wamesaini mkataba wa kutoa huduma za
afya kwa wanachama wa mpango wa uchangiaji wa hiari leo jijini Dar es
Salaam
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), Michael
Mhondo wakushoto na kulia ni Mkurugenzi wa PSPF Adam Maingu, wakisaini
mkataba wa kutoa huduma za afya kwa wanachama wa mpango wa uchangiaji
wa hiari. leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), Michael
Mhondo na Mkurugenzi wa PSPF Adam Maingu,wakishikana mikono baada ya
kusainiwa mkataba huo
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), Michael
Mhondo na Mkurugenzi wa PSPF Adam Maingu, wakizidua huduma za afya kwa
wanachama wa mpango wa uchangiaji wa hiari. leo jijini Dar es Salaam.
MFUKO
wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma(PSPF) kwa kushirikiana na Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), wamesaini mkataba wa kutoa huduma za afya
kwa wanachama wa mpango wa uchangiaji wa hiari.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa PSPF Adam Maingu alisema idadi
kubwa ya wanachama wa uchangiaji wa hiari ni watanzania ambao wapo
katika sekta binafsi na sekta isiyo rasmi kama waendesha bodaboda,
mamalishe, wakulima, wafugaji, wasanii, wanamichezo na wajasiriamali.
Amesema
baada ya kufanya utafiti waligundua kuwa matatizo makubwa
yanayowakabili ni upatikanaji wa huduma za afya hivyo wamekubaliana na
mfuko wa bima ya afya kwamba mwanachama atakayelipia kiasi cha Sh
76,800 atatengenezewa kadi ya bima ya afya na atapata huduma za afya
kwa kipindi cha mwaka mmoja chini ya udhamini wa PSPF.
“Walengwa
wakuu katika fao hili la matibabu ya PSPF ni wanachama wa Mpango wa
Uchangiaji wa Hiari na wategemezi wao watano kwa kila mwanachama.
“Mwanachama
wa PSPF atakayejiunga na mpango huo atanufaika na mafao yote ya bima
ya afya sawasawa na mwanachama mwingine yeyote wa Mfuko wa Taifa wa
Bima ya Afya.
“Huu
ni mpango wa aina yake katika sekta ya Hifadhi ya Jamii hapa nchini,
kwani mnufaika atapatiwa kadi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na
kuweza kupatiwa huduma ya matibabu nchi nzima kwenye vituo vyote
vilivyosajiliwa na NHIF kuanzia Hospitali ya Taifa, rufaa, Hospitali za
binafsi, mikoa, vituo vya afya na zahanati zote za Serikali.
“Pia
huduma hiyo itakuwepo katika vituo vya mashirika ya dini na binafsi
pamoja na maduka ya dawa yaliyosajiliwa na PSPF,”alisema Maingu.
Kwa
upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Michael
Muhando, alisema kusainiwa kwa mkataba huo utawanufaisha wananchi
wengi waliojiunga katika vikundi mbalimbali vya ujasiriamali vikiwemo
vya umoja wa madereva wa malori, wavuvi, wakulima pamoja na vyama vya
waandishi wa habari.
“Lengo
ni kuwajengea uwezo wajasiriamali kuwa na maisha bora, na vikundi 38
tayari tumeshavisajili na mfumo wa awamu ya tano wa ‘Hapa kazi tu’
tunautekeleza kwa kasi” alisema Muhando.
Comments