YANGA SC WAWASILI PEMBA KWA KAMBI YA 'KUUWA MNYAMA' JUMAMOSI TAIFA


Wachezaji wa Yanga SC, baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Zanzibar tayari kuunganisha ndege kwenda Pemba kuweka kambi ya kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya mahasimu wa jadi, Simba SC Jumamosi ijayo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga SC, Jerry Muro tayari kikosi cha Yanga SC kipo Pemba na kesho kitaanza mazoezi kwenye Uwanja wa Gombani
Yanga SC iliondoka Dar es Salaam Ijumaa Saa 1:00 usiku kwenda Mauritius kabla ya leo kutuan Zanzibar
Yanga SC iliwasili Zanzibar majira ya Saa 4:00 asubuhi na hadi Saa 6:00 mchana, tayari walikuwa Pemba
Yanga SC jana ilishinda 1-0, Mauritius, bao pekee la Mzimbabwe Donald Ngoma dhidi ya wenyeji Cercle de Joachim katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika na timu hizo zitarudiana wiki mbili zijazo Dar es Salaam

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.