NAIBU WAZIRI ANNASTAZIA ATOA MAAGIZO KIWANJA CHA TBC KILICHOPO KIMANI WILAYA YA KISARAWE KUPATIWA HATI


KISA1
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Annastazia Wambura akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Bi Nahya Mansour alipowasili katika Ofisi za Wilaya hiyo kwa ziara ya kikazi ya kukagua Viwanja vya makazi vya Shirika la Utangazi  Tanzania (TBC) vilivyopo wilayani humo.
KISA2
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Annastazia Wambura akizungumza na viongozi wa Wilaya ya Kisarawe(Hawapo pichani) alipofika katika ofisi za Wilaya hiyo kwa ajili ya ziara ya kikazi.
KISA3
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Annastazia Wambura akipokea taarifa ya kiwanja cha Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kilichopo eneo la Kimani katika Wilaya ya Kisarawe kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo Bi Mwanamvua Mrin
KISA4
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Annastazia Wambura akitoa maelekezo kwa Meneja Miradi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Bw. Mackselin Chota.
…………………………………………………………………………………………………………..
Na Shamimu Nyaki, WHUSM
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura amemuagiza Meneja wa Miradi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC ) Bw. Mackselin Chota kuhakikisha kiwanja  Na.1 Kitalu “B” kilichopo eneo la Kimani wilaya ya Kisarawe kinapatiwa Hati Miliki  ili kuepusha kuvamiwa pamoja na migogoro inayoweza kutokea.
Agizo hilo amelitoa jumamosi wakati alipotembelea kiwanja hicho na kueleza kuwa kiwanja hicho ni lazima kiendelezwe kwa ajili ya kuwasaidia wafanyakazi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ambapo kiwanja hicho kilitafutwa kwa dhumuni hilo.
“Naishukuru Halmashauri kwa  kutoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo,hivyo natoa siku saba kwa  idara ya Miradi ya TBC kushirikiana na Halmashauri kuhakikisha kiwanja hicho  kinapatiwa Hati”.Alisema Mhe.Annastazia.
Aidha amewataka kuwasilisha gharama zilizotumika katika ujenzi wa nyumba zilizopo katika eneo hilo na wapi zimetoka na sababu zilizosababisha ujenzi huo kukwama kwa zaidi ya miaka mitatu.
Akitoa maelezo kuhusu Kiwanja hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Bi Mwanamvua Mrindoko amesema kuwa kiwanja hicho kilipimwa  na ramani yake ya upimaji ilipata kibali cha Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi na kusajiliwa kwa namba 68480,ramani namba E 292/83 ya tarehe 22 februari, 2012.
“Taratibu za umilikishwaji zilifanyika kwa kuandaliwa gharama za kulipia kabla hati haijaandaliwa,malipo hayo yalifanywa na TBC kupitia NMB na kuwasilisha fomu ya malipo hayo(Bank pay in slip)”.Alisema Bi Mwanamvua.
Naye Meneja wa Miradi wa Shirika la Utangazaji Tanzania  Bw.Mackselin Chota amesema kuwa Shirika hilo lina jumla ya viwanja 55 nchi nzima,ambavyo 19 kati ya hivyo vina Hati miliki ambapo katika mkoa wa Pwani kuna kiwanja kimoja, Dar es Salaam viwanja vitano ambavyo viko Pugu Road,Kunduchi, na TAZARA, Mikocheni na Sinza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.