KAMPUNI YA VISION INVESTIMENTS YATOA FURSA KWA MAKAMPUNI MENGINE.



Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Vision Investiments Ally Nchahaga (katikati) akifafanua juu ya fursa zitolewazo na Kampuni yao leo Jijini Dar es Salaam, kulia ni Afisa Mahusiano wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Aisha Mohammed na kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mauzo cha Kampuni ya Mafuta ya Oil com Aluwy Amar.

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO

Kampuni ya Vision Investments imetoa fursa kwa makampuni mengine kushiriki kutoa huduma mbalimbali wakati wa makutano baina ya wanunuzi na wauzaji wa magari yanayoandaliwa na Kampuni hiyo yatakayofanyika Mei 29 mwaka huu.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Ally Nchahaga ambaye amewaomba wauzaji na wanunuzi wa magari pamoja na makampuni mbalimbali kushiriki katika makutano hayo ili kutimiza mahitaji yao ya magari.

“Kama ilivyo ada kila Jumapili ya mwisho wa mwezi Kampuni yetu inawakutanisha wauzaji, wanunuzi wa magari pamoja na makampuni tofauti kutoa huduma shirikishi zinazokwenda sambamba na biashara hii ya magari ya watu binafsi” alisema Nchahaga.Kwa mujibu wa Kampuni ya Vision Investments makutano hayo yatafanyika nchini kwa mara ya sita ambapo mwaka huu yatafanyika katika viwanja vya Coco Mihogo kuanzia sa 4 asubuhi.

Nchahaga alizitaja baadhi ya kampuni zinazotoa huduma shirikishi zikiwemo Benki ya watu wa Zanzibar (PBZ), Kampuni ya Mafuta ya Oil com, Kampuni ya Coca cola, pamoja na Kampuni ya Simply Elegant ambazo zinatoa huduma za mikopo ya magari, mafuta ya magari, vinywaji pamoja na vilainishi vya magari kwa wateja watakaokuwepo katika makutano hayo.

Aidha, Nchahaga amesisitiza kuwa kampuni yao sio ya maonyesho ya magari wala wao sio madalali bali ni kampuni inayotoa fursa yenye gharama nafuu kwa wanachi kutimiza mahitaji yao ya magari.

Ameongeza kuwa elimu kuhusu magari na vifaa vyake itatolewa bure na mtu yeyote atakayehitaji kuuza gari lake atachangia shilingi elfu 50 ikiwa ni mchango wa kuweka gari lake katika viwanja hivyo pamoja na kufanyiwa matangazo katika mitandao ya kijamii kwa mwezi mzima.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Mauzo cha Kampuni ya Mafuta ya Oil com Aluwy Amar amesema kuwa Kampuni yao inatoa huduma mpya ya kulipa kwa kutumia kadi itakayomrahisishia mteja kupatiwa huduma za mahitaji ya mafuta ya magari yao kwa hiyo, watashiriki katika makutano hayo ili kutoa elimu kwa wateja hao kuhusu matumizi ya kadi hizo.

“Huduma hii tumeianza kuitoa kwa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, huduma za kupatiwa kadi pamoja na kufanya miamala yote ni bure pia mwisho wa mwezi tutatoa huduma ya punguzo la bei kulingana na matumizi ya mteja”,alisema Amar.

Kwa upande wake Afisa Mahusiano wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Aisha Mohammed amesema kuwa wamefurahi kupata fursa hii ya kushiriki katika makutano hayo kwakua anaamini ni njia moja wapo kwa benki hiyo kuwapa mikopo au kuwanunulia magari wateja wao ili kutimiza ndoto zao kwa muda muafaka.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.