Ombi la kutaka shamba hilo lichukuliwe lilitolewa na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Julius Karanga (Chadema), wakati akichangia majadiliano ya makadirio ya Bajeti ya wizara hiyo, bungeni Dodoma leo.
Waziri Lukuvi, amejibu kuwa serikali imesikia kilio chako na cha wananchi wa Monduli kuhusu shamba hilo na kwamba sasa shamba hilo ambalo wakati wa Rais Benjamin Mkapa lilitaifishwa kutoka kwa Mfanyabiashara Stein na kuamuru ligawiwe kwa wananchi lakini lilichukuliwa na Lowassa.
Amesema kama Mheshimiwa Mbunge, Karanga alikuwa hajui kwamba shamba hilo la makuyuni alijimilikisha Lowassa, basi imekula kwake, shamba linachukuliwa na serikali na kuligawa kwa wananchi. Najua kazi ni ngumu kwako, lakini naomba tushirikiane shamba hili liende kwa wananchi.
"Ninayo hati hapa ya shamba hilo imesainiwa na Lowassa, nasema tutairekebisha ili shamba hilo ligawiwe kwa wananchi." alisema Lukuvi huku wabunge wengine wakicheka.
Alisema kuwa wakati shamba hilo anajilimikisha. Lowassa alikuwa waziri wa nchi ofisi ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
Comments