MWENGE WATUA IRINGA LEO



Mkuu  wa  wilaya ya  Iringa Richard  Kasesela  akipokea mwenge  wa  Uhuru  kutoka kwa  mkuu mkuu ya  Mufindi  Bw  Jowika  Kasunga  leo baada  ya  kuanza mbio  zake  wilaya ya  Mufindi
Mbio za  Mwenge  katika Halmashauri ya  Iringa
Mkuu  wa  wilaya ya  Iringa Richard  kasesela wa  tatu  kulia  akisakata  dansi  katika mapokezi ya  Mwenge Iringa
HALMASHAURI  za  wilayani  nchini  zimetakiwa  kutenga   pesa za  makusanyo  ya  ndani  kwa ajili ya  kuwasaidia  vijana asilimia  tano ya  makusanyo  hayo ili  kutumika kuwakomboa vijana  kiuchumi .

Rai  hiyo  imetolewa  leo na  kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, George Mbijima wakati  wa  mkesha  wa  mbio hizo mwenge  kijiji  cha  Ifunda katika  halmashauri ya  wilaya ya  Iringa .

Alisema  kuwa  jukumu  ya  Halmashauri  kutenga  asilimia 5 ya makusanyo yake  ya mapato  ya  tayari  serikali  imeagiza kufanya  hivyo  na  ni vema kila Halmashauri  kuhakikisha inatenga   fedha  hizo  kwa  ajili ya vijana ikiwa ni  pamoja na kuwatengea  ardhi  kwa  ajili ya  kufanyia  shughuli  za kiuzalishaji .

Mbijima alisema “rai yangu kwenu vijana ni kutoa nguvukazi kwa kushiriki kwa moyo thabiti katika kazi za ujenzi wa miradi ya maendeleo. Kufanya hivyo kutasaidia kuharakisha ukamilishaji wa miradi hiyo. Aidha, nawapongeza kwa utayari wenu kwa mradi huu wa maji na kuchangia asilimia 2.5 ya gharama za mradi huu wa maji”.

Kiongozi huyo aliwahakikishia wananchi wa vijiji hivyo kuwa Ofisi ya Rais, Tawaala za Mikoa na Serikali za Mitaa pamoja na Halmashauri ya wilaya ya  Iringa  zitaendelea kutafuta fedha za kukamilisha mradi huo muhimu.

Alisema lengo la Serikali ni kuendelea kusogeza huduma ya maji kwa wananchi kama Sera ya Maji ya mwaaka 2002 inavyoelekeza.

Huku  akiwataka  vijana kuacha  kutumia  fedha hizo  za  mikopo kuongeza  wake  ama  kufanyia  anasa  zisizo na tija katika maisha  yao.

Alisema  Miradi mbali mbali ambayo  imezinduliwa  kwa  ajili ya  vijana ukiwemo mradi wa  kilimo kwa  kijiji cha  Usengelendeti kwa  ajili ya  kikundi cha vijana  wa Nguvu kazi ambao  wanafanya  shughuli ya  kilimo ni  moja kati ya  miradi itakayowakomboa  vijana   iwapo  watatimiza  wajibu wao.

Akisoma  risala  ya  utii kwa  Rais wa Dr  John Magufuli wakati wa  hitimisho ya  mbio  hizo kwenye  halmashauri ya  wilaya ya  Iringa mkuu  wa  wilaya ya  Iringa Bw  Richard  Kasesela  alisema  kuwa  katika  kuwajali  vijana  jumla  ya mikopo kwa vikundi  vya vijana  vya  kijasiliama mali vikundi 38  vimepatiwa  mikopo yenye thamani ya  Tsh milioni 60.2 kwa  ajili  ya  vikundi  zimetolewa kati  ya  fedha  hizo Tsh  milioni 37.5 zilitokana  na asilimia  5 ya mapato  ya  ndani  na  Tsh milioni 17.7 zilitokana  na mfuko  wa vijana wa  Halmashauri  huku  Tsh .milioni 5 iliokana  na mkopo wa wizara  ya habari ,vijana  utamaduni na michezo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.