Waziri wa kilimo ,Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba ambae ni mbunge wa jimbo la Iramba akiwapungia mikono wananchi wa Morogoro wakati akiwasili katika viwanja vya Ndege kuzindua tamasha la Urafiki |
Waziri Nchemba akimsikiliza mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren |
mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akiwa katika picha ya pamoja na waziri wa kilimo ,Mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba |
Waziri Nchemba akipokelewa na RC Morogoro Dkt. Kabwe Steven Kabwe |
Waziri Nchemba akiwasili uwanja wa mkutano |
mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt. Kabwe Steven Kabwe kulia akiwa na waziri Nchemba |
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt. Kabwe Steven Kabwe kulia akimwongoza waziri Nchemba |
mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akiteta jambo na waziri Nchemba |
Mapokezi ya waziri Nchemba Morogoro |
Kwaya ikitumbuiza katika uwanja huo |
Waziri Nchembe akizindua tamasha hilo |
W |
mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akiendelea kuhubiri |
Wananchi wakiwa katika viwanja hivyo |
Mtoto ambae alikuwa hasikii toka azaliwe akijaribiwa baada ya kuombewa na kupona |
Mwanamke aliyekuwa kapooza akitembea baada ya maombi |
Mmoja kati ya watu walioanguka kwa mapepo uwanjani wakati wa maombi |
Mwanamke ambae alikuwa na matatizo ya kusikia kwa miaka zaidi ya 15 akitoa ushuhuda baada ya kuombewa na mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren kushoto |
mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akihubiri katika tamasha la Urafiki mjini Morogoro |
“ Tunapokusanyika na
tunapokuwa faragha katika
ibada zetu tuliombee taifa letu ……jambo la pili kwa uzito
huo huo tumwombee Rais wetu mpendwa Dr John Magufuli kazi anayoifanya ni ngumu … kazi anayoifanya
ni kwa niaba ya watanzania wote na utashi ule anaoendanao ninyi wenyewe
mliomba sana kabla ya kumpigia
kura ….uzoefu unaonyesha mabadiliko huwa
hayaji rahisi rahisi adui
huwa hakubali kushindwa kirahisi
kwa hiyo
kila tunapoongea na Mungu
wetu tukumbuke kumwombea Rais wetu ili kila mema
anayoliwazia Taifa yaweze kutimia” alisema waziri Nchemba
Kuwa kwa upande wake
kila anapoona watumishi wa Mungu
wakiwa wamekusanyika kwa ajili ya huduma huwa haachi kuwasogelea
japo kushikana nao mikono kama sehemu ya
kupokea baraka kutoka kwao
kwani wapakwa mafuta wakisema
tu ubarikiwe Mungu juu mbinguni
huweka tiki ya baraka.
“Na hivyo ndivyo
nilivyopata hata ubunge
nilikuwa sina gari wala baiskeli na
wazazi wangu walikuwa wanaishi katika nyumba
ya tembe wakiwa na maisha magumu nikaenda kanisani kulikuwa na Harambee japo sikuwa na pesa nyingi
niliamua kuchangia kidogo
tu …..watumishi wale
wakasema Ee Mungu mjalie haja ya
moyo wake huyu kijana na mimi nilikuwa nikiwaza ubunge kweli ubunge ukatiki …..na
hivi leo amekuja mhubiri wa
kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akasema kwa lugha ya kiingereza kuwa Ee Mungu timiza ndoto ya
kijana huyo na mimi ndogo hiyo inaendelea kuota
hivyo hivyo kwa hiyo najua na ninyi mtanikumbuka katika
majukumu ambayo nimepewa na Rais ……leo
baada ya saa 4 asubuhi hatukuwa na ratiba ya vikao vya bunge
nimelazimika kuja Morogoro kuifanya kazi hii na leo hii nitageuza
bungeni “
Kwani alisema
majukumu ambayo anayatumikia pia yana harufu
ile ile ya ambayo amewaomba kuzidisha
maombi kuliombea Taifa kwani yana harufu ya umwagaji wa damu .
Alisema waziri Nchemba kuwa alipoteuliwa na Rais Dr Magufuli
kabla hata ya kuapishwa alipata taarifa ya mifugo kuuwawa na
watu kuchinjana kwa kukatana
mapanga mkoani Morogoro ambayo yalimkumbusha mapigano ya chuki na wivu kwa Abeli na Kaini mmoja akiwa mkulima na
mwingine mfugaji .
“ Tuliombee Taifa
letu kila mmoja afanye kazi
inayomlete kipato pasipo kuwa na wivu na
bila kuwa na dharau kwa kazi ya mwenzake ….kila nikipita
huwa nawaeleza watumishi
wangu kuwa hakuna mali ,mifugo,shamba ama kitu chochote chenye dhamani kubwa
kuliko uhai wa mwa wanadamu”
Kuwa serikali itatengeneza mazingira bora
ya wakulima ama wafugaji kufanya kazi
zao kwa uhuru na amani japo
kila mmoja anapaswa kutambua
kuwa uhai ni zaidi ya yote.
Kwa upande wake mhubiri
wa huyo kimataifa toka nchini
Canada Dr Peter Youngren limpongeza waziri Nchemba kwa
kujiweka mbele katika huduma&nbs
...
Comments