Mkuu wa wilaya ya Kakonko Col. Hosea Maloda Ndagala akikabizi funguo za magari mawili ya kubebea wagonjwa (hayapo pichani)kwa Mganga Mkuu wa kituo cha afya Mgaza Wilayani Kakonko Dkt Selemani Fadhiri. Wanaoshuhudia wapili kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya KakonkoLusubilo Mwakabibi na kushoto ni Diwani wa Kiziguzigu, Renatus Daniel.
Mkuu wa Wilaya akijaribu moja ya ma Mkuu wa Wilaya akijaribu moja ya magari hayogari hyo.
Mkuu wa Wilaya ya Kakonko, Col. Hosea Ndagala akiongea na Madiwani. Watumishi wa Hospital wakati wa hafla ya kukabidhi magari ya wagonjwa katika kituo cha afya Mgaza Wilayani Kakonko
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kakonko akitoa shukrani wakati wa hafla ya kukabidhi magari hayo.
**********
Cosmas Makalla, Kakonko
MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Maloda Ndagala amekabidhi magari mawili mapya ya kubebea wagonjwa aina ya Toyota Land Cruiser Hard top Ambulance yenye thamani ya dola za kimarekani 18,000 kwa gari moja kwa vituo vya afya viwili Wilayani Kakonko hivi karibuni.
Kanali Hosea Ndagala ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla iliyofanyika katika kituo cha afya Mganza amesisitiza magari hayo kutumika kubebea wagonjwa kama ilivyokusudiwa.
“Naagiza magari haya ya wagonjwa yatumike vizuri kwa kubebea wagonjwa hasa wanawake wanaokwenda kujifungua na kutunzwa vizuri ili baada ya miaka mitano ya mkopo yaonekane yakiwa katika hali nzuri
Comments