NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
RAIS wa pili na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Serikali ya Zanzibar, Mzee Aboud Jumbe Mwinyi, (96), amefariki dunia leo Agosti 14, 2016.
Mwinyi ambaye alikuwa akiishi Mji Mwema Kigamboni jijini Dar es Salaam, tangu patokee “mchafuko wa hali ya hewa” kisiwani Zanzibar, alikuwa akisumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu.
Hayati Jumbe alianza kuitawala Zanzibar mnamo Aprili 11, 1972 mara baada ya kuuawa Rais wa Kwanza wa visiwa hivyo, Hayati Mzee Abeid Aman Karume Aprili 7, 1972.
Mzee Jumbe alitawala visiwa hivyo tangu wakati huo hadi Januari 30, 1984 alipojiuzulu kufuatia msimamo wake wa kutaka mabadiliko katika mfumo wa Muungano wa baina ya Zanzibar na Tanzania bara.
Mzee Mwinyi alizaliwa Juni 14, 1920
Mwenyezimungu ailaze roho yake mahala pema peponi AMIN
Comments