WAZIRI WA AFYA MHE UMMY MWALIMU AKUTANA NA BALOZI YA ISRAEL


 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akizungumza na Balozi wa Israel nchini Tanzania anayezihudumia pia nchi Afrika Mashariki za Kenya na Uganda Mhe. Yahel Vilan (kulia) Ofisini kwake leo jijini Dar es salaam. Pamoja na mambo mengine viongozi hao wamejadili kuhusu uanzishwaji wa ushirikiano katika maeneo mbalimbali yatayoinufaisha Tanzania na Israel kwenye sekta ya Afya.
Balozi wa Israel nchini Tanzania anayezihudumia pia nchi Afrika Mashariki za Kenya na Uganda Mhe. Yahel Vilan (kulia)akimweleza jambo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu mara baada ya kumtembelea Ofisini kwake leo jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu (katikati) akifurahia jambo mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo baina yake na Balozi wa Israel nchini Tanzania anayezihudumia pia nchi Afrika Mashariki za Kenya na Uganda Mhe. Yahel Vilan (kulia) Ofisini kwake leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mafunzo ya Wizara hiyo, Agnes Kimemio.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiagana na Balozi wa Israel nchini Tanzania anayezihudumia pia nchi Afrika Mashariki za Kenya na Uganda Mhe. Yahel Vilan (kulia) mara baada ya mazungumzo Ofisini kwake leo jijini Dar es salaam.Picha/Aron Msigwa -MAELEZO.


Na. Mwandishi Wetu - Dar es Salaam.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Israel nchini Tanzania Mhe. Yahel Vilan ambapo pamoja na mambo mengine viongozi hao wamekubaliana kuanzisha ushirikiano katika maeneo mbalimbali ambayo yatazinufaisha Tanzania na Israel katika sekta ya Afya.


Balozi huyo anayezihudumia nchi za Afrika mashariki Tanzania, Kenya na Uganda katika mazungumzo na Waziri wa Afya wa Tanzania Mhe. Ummy Mwalimu ameyataja baadhi ya mambo ambayo Israel imekua ikishirikiana na Tanzania kuwa ni pamoja na kudhamini matibabu ya moyo kwa Watoto kupitia Taasisi ya Save Child Heart ya Israel na Mafunzo ya madaktari bingwa na Wauguzi kutoka Hospitali mbalimbali nchini.

"Tumekuwa na utaratibu wa kuleta madaktari ili waje watoe huduma kwa wagonjwa pamoja na ujuzi kwa wataalam wa Tanzania" Ameeleza Balozi Vilam na kuongeza kuwa Israel imekuwa ikitoa mafunzo ya muda mfupi kwa wataalam kutoka Tanzania hususani madaktari na Wauguzi.

Balozi huyo amesema kuwa Israel imekua ikitoa mafunzo ya muda mfupi kwa wataalam hususani madaktari na Wauguzi kutoka Tanzania na kuongeza kuwa wanao mpango wa kusaidia uanzishwaji wa chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) katika eneo ambalo serikali ya Tanzania itapenda kuboresha huduma hiyo.

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu ameishukuru Serikali na Wananchi wa Israel kwa ushirikiano wanaouonyesha kwa Tanzania katika eneo la tiba hususani kwenye udhamini wa matibabu ya watoto wenye ugonjwa wa moyo katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kupitia madaktari bingwa wanaotoka katika nchi mbali mbali ikiwemo Israel.


"Kupitia ushirikiano na Israel, Serikali tumeweza kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambazo zingetumika kupeleka wagonjwa nje ya nchi kwa matibabu, hadi sasa kati ya wagonjwa 400 waliokuwa wanasubiri kupelekwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu nusu yao wamepatiwa matibabu hapa nchini chini ya utaratibu huo". Ameeleza Mhe Ummy.



Mhe. Ummy amemwomba Balozi wa Israel kuongeza  fursa zaidi za mafunzo ya fani ya Afya kwenye kada nyingi zaidi ikiwemo kada ya wataalam wa maabara, wauguzi na madaktari.


Aidha, amemwomba Balozi wa Israel kuwezesha ujenzi wa chumba cha wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Benjamin Mkapa - Dodoma.


 Amesema hatua hiyo inatokana na uamuzi wa serikali kuhamia Dodoma ambapo maboresho makubwa ya utoaji wa huduma za afya yanatakiwa ili kuweza kuhudumia watu watakaohamia Dodoma.

Akikubali ombi hilo, Balozi wa Israel Mhe. Yahel Vilan ameeleza kuwa wataalam kwa ajili ujenΕΊi wa chumba cha wagonjwa mahututi wanatarajia kufika nchini Tanzania mwezi Septemba kwa ajili ya kuendelea na utekelezaji wa ahadi ya balozi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.