AZAM YAPIGWA NA NDANDA 2-1


Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
NDANDA FC imewaangusha washindi wa Ngao ya Jamii Azam FC kwa mabao 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Nangwanda SIjaona, Mtwara leo.
Mabao ya Ndanda yamefungwa na Riffat Khamis na Hajji Mponda, wakati la Azam FC lilifungwa na Nahodha John Raphael Bocco.
Hicho kinakuwa kipigo cha pili mfululizo kwa Azam FC baada ya wiki iliyopita kufungwa 1-0 na Simba SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
Matokeo hayo yanaifanya Azam FC ibakie na pointi zake 10 baada ya kucheza mechi sita, wakifungwa mbili, sare moja na kushinda tatu.
Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, JKT Ruvu wameshinda 2-0 dhidi ya Mbeya City Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani, Prisons wametoka sare ya 0-0 na Mwadui Uwanja wa Sokoine, Mbeya na Mtibwa Sugar imelazimishwa sare ya 1-1 na Mbao FC Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.
Ligi Kuu inaendelea kesho kwa mechi mbili; Ruvu Shooting na Toto Africans Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani, Stand United na Yanga SC Uwanja wa Kambarage, Shinyanga na kesho African Lyon itamenyana na Kagera Sugar Uwanja wa Taifa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI