Assist ya Samatta imeinusuru KRC Genk na kipigo cha tano msimu huu


Baada ya watanzania kupokea good news ya nahodha wao wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Mbwana Samatta kuteuliwa katika list ya majina 30 ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora Afrika 2016, nyota huyo usiku wa October 15 alishuka dimbani kuisaidia timu yake ya KRC Genk kuwania point tatu ugenini dhidi ya Mouscron.
Samatta ambaye alianzia benchi na kuingia kipindi cha pili dakika ya 67 kuchukua nafasi ya mjamaica Leon Bailey, alishuhudia timu yake ya KRC Genk ikiwa nyuma kwa goli 2-1 hadi alipoingia kwenda kuongeza nguvu dakika ya 78 akafanikiwa kutoa assist na kuinusuru KRC Genk isipoteze mchezo wa tano wa Ligi Kuu Ubelgiji msimu huu.
Kufuatia matokeo hayo KRC Genk inakuwa nafasi ya 9 katika msimamo wa Ligi KuuUbelgiji, magoli ya KRC Genk yote yalifingwa na mgiriki Nikolaos Karelis dakika ya 33 baada ya kutumia vyema pasi ya Pozuelo na 78, wakati magoli ya Mouscron yalifungwaHassan Mahmoud dakika ya 3 na Valentin Viola dakika ya 42.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.