AZAM FC WATUA BUKOBA KUIONGEZEA MACHUNGU KAGERA SUGAR


Na Mwandishi Wetu, BUKOBA
KIKOSI cha Azam FC, kimetua salama saa 8 mchana mjini Bukoba, mkoani Kagera kikiwa na kazi moja tu ya kusaka pointi tatu muhimu katika mchezo ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) utakaofanyika kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini humo Ijumaa ijayo.
Wachezaji wa Azam FC pamoja na benchi la ufundi wameonekana kuwa na morali kubwa kuelekea mchezo huo, utakaofanyika katika uwanja ambao unafanana na ule wa Azam Complex unaotumiwa na matajiri hao, kutokana na vyote kuwa na nyasi bandia.
Mara baada ya kikosi hicho kuwasili mjini humo na kufikia katika Hoteli ya Smart, Kocha Mkuu wa Azam FC, Zeben Hernandez, ameweka wazi kuwa mipango yao ni kuibuka na pointi tatu hukua akieleza programu yake kwa ujumla kuelekea kipute hicho.
Hernandez amewapa mapumziko ya siku ya leo nyota wake kutokana na uchovu wa safari ndefu ya siku mbili, iliyoanzia jana alfajiri na kisha kupumzika mjini Kahama Shinyanga kabla ya leo asubuhi kuanza safari ya takribani saa sita na kuwasili mjini hapa.
Kwa mujibu wa programu ya Hernandez, kikosi hicho kitaanza kufanya mazoezi kesho kwa vipindi viwili (asubuhi na jioni) kabla ya Alhamisi kujifua kwa mara ya mwisho jioni kabla ya kupambana na Kagera Sugar ambayo imetoka kufungwa mabao 6-2 na Yanga Jumamosi iliyopita huku mabingwa hao wakiichapa JKT Ruvu bao 1-0.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.