Taasisi za umma zatakiwa kuhuisha taarifa katika Tovuti zao


Mkurugenzi wa Idara ya Habari, MAELEZO Bw. Hassan Abbas akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu taasisi za Serikali kutekeleza agizo la kuhuisha taarifa na huduma katika Tovuti zao mapema kabla ya mwisho wa mwezi huu katika mkutano uliofanyika Ofisi za Wakala ya Serikali Mtandao (EGA) leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala ya Serikali Mtandao Bibi. Susan Mshakangoto. 

Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala ya Serikali Mtandao Bibi. Susan Mshakangoto akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa mkutano na waandishi hao leo jijini Dar es Salaam, kuhusu taasisi za umma kuhuisha taarifa katika Tovuti zao. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari, MAELEZO Bw. Hassan Abbas. 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari, MAELEZO Bw. Hassan Abbas akiwaonyesha waandishi wa habari mwongozo wa utengenezaji wa Tovuti za Serikali wakati wa mkutano wake na waandishi hao leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala ya Serikali Mtandao Bibi. Susan Mshakangoto. 
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wao na Mkurugenzi wa Idara ya Habari, MAELEZO Bw. Hassan Abbas na Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala wa Serikali Mtandao (EGA) Bibi. Suzan Mshakangoto (hawapo pichani). Mkutano huo ulihusu kuzikumbusha Taasisi za umma kuhuisha taarifa katika Tovuti zao leo Jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari, MAELEZO Bw. Hassan Abbas akielezea namna ambazo mitandao ya kijamii inavyo tumika kurahisisha kufikisha taarifa za Serikali kwa jamii na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu taasisi za umma leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala ya Serikali Mtandao, Bibi. Susan Mshakangoto. Mkurugenzi huyo alitolea mfano wa akaunti ya Tweeter ya, Msemaji wa Serikali@ TZ_Msemaji Mkuu. Mwananchi anaweza kuifuata akaunti hiyo kwa kutafuta “Msemaji Mkuu wa Serikali on Twitter”.

Picha na: Frank Shija, MAELEZO

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.