TAMBWE YUKO FITI KUIVAA AZAM JUMAPILI


Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
MSHAMBULIAJI tegemeo la mabao la Yanga SC, Amissi Tambwe anatarajiwa kuendelea na mazoezi kesho kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Jumapili.
Mpachika mabao huyo wa Burundi, aliumia dakika ya 87 jana baada ya kugongana na kiungo wa Mtibwa Sugar, Shaaban Nditi na kupasuka juu ya jicho, hivyo kushindwa kuendelea na mchezo.
Hata hivyo, Yanga iliyokuwa imemaliza nafasi za kubadilisha wachezaji, ilimalizia pungufu na kufanikiwa kuulinda ushindi wa 3-1.
Amissi Tambwe anatarajiwa kuendelea na mazoezi kesho kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Jumapili

Lakini Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh ameiambia BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE leo kwamba kinara huyo wa mabao wa wana Jangwani hao anaendelea vizuri na kesho ataanza mazoezi.
Yanga sasa inaelekeza nguvu zake kwenye maandalizi ya mchezo ujao baada ya ushindi wa 3-1 jana mbele ya Mtibwa. 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.