SIMBA B YAANZA NA MOTO LIGI YA VIJANA


Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
TIMU ya Simba imeanza vyema Ligi Kuu ya Vijana chini ya umri wa miaka 20 Tanzania Bara baada ya kuifunga Ndanda FC ya Mtwara mabao 2-1 katika mchezo kituo cha Dar es Salaam.
Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam, mabao ya Simba yalifungwa na Rashid Juma dakika ya 24 na Moses Kitandu dakika ya 57, wakati la Ndanda limefungwa na Joseph Hilly dakika ya 89 kwa penalti. 
Mashabiki wa Simba wanafurahia timu zao kufanya vizuri katika Ligi ya Bara

Katika mchezo uliofuatia Ruvu Shooting wameilaza 1-0 JKT Ruvu Uwanja wa Azam Complex pia. Bao pekee la Ruvu limefungwa na Salehe Likwayu dakika ya 62 kwa mkwaju wa penati baada ya William Patrick kuchezewa rafu.
Mechi ya ufunguzi jana, Yanga ilitoa sare ya 1-1 na wenyeji Kagera Sugar kituo cha Bukoba, Uwanja wa Kaitaba na kesho jioni Chamazi Majimaji itamenyana na Mtibwa Sugar.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.