SIMBA NA YANGA MARUDIANO FEBRUARI 18...MZUNGUKO WA PILI WAANZA WIKI IJAYO


Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
MZUNGUKO wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara unatarajiwa kuanza Desemba 17, mwaka huu wakati mchezo wa mahasimu wa jadi, Simba na Yanga utakuja Februari 18, mwakani.
Baada ya mapumziko ya tangu Novemba 10, kufuatia kumalizika kwa mzunguko wa kwanza kitimutimu cha Ligi Kuu kinarejea Jumamosi ya Desemba 17, mabingwa watetezi, Yanga SC kufungua dimba na JKT Ruvu Stars Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Mechi nyingine siku za siku hiyo, Mbeya City watamenyana na Kagera Sugar Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, Mwadui na Toto Africans Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga na Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani.
Vinara wa ligi hiyo, Simba wataanza kampeni ya kuwania taji la kwanza baada ya miaka minne Jumapili ya Desemba 18 watakapoifuata Ndanda Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, siku ambayo Mbao FC watamenyana na Stand United Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, African Lyon na Azam Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na Prisons na Maji Maji Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.